Utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea upande wa mashariki. Pamoja nao kulikuwa mushindo wa kuja kwake kama mushindo wa maji mengi, inchi ilingaa kwa utukufu wake.
Halafu mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe saba akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha namna gani yule kahaba mukubwa atakavyohukumiwa, ndio ule muji uliojengwa katikati ya mito mingi.
Kisha nikaona malaika mwingine mwenye uwezo akishuka toka mbinguni. Alikuwa akifunikwa na wingu, naye alikuwa na upindi wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingaa kama jua na miguu yake ilimetameta kama nguzo ya ndimi za moto.
Halafu yule malaika akaniuliza: “Kwa nini unashangaa? Nitakuambia maana ya fumbo la mwanamuke yule na ya yule nyama anayemubeba, na anayekuwa na vichwa saba na pembe kumi.