Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 16:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Malaika wa tano akamwanga kikombe chake juu ya kiti cha kifalme cha yule nyama wa ajabu, na ufalme wake ukafunikwa na giza. Watu wakaanza kutafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 16:10
22 Referans Kwoze  

Nyota ile ikafungua hilo shimo. Moshi unaokuwa kama moshi wa furu kubwa ukapanda toka ndani ya shimo lile. Giza la ule moshi uliotoka ndani ya lile shimo ulifunika jua na anga.


Lakini wale waliopaswa kushiriki katika Ufalme ule watatupwa inje kwenye giza, na kule watalia na kusaga meno.”


Mwangaza wa taa hautaonekana tena ndani yako. Na hakutasikilika tena kelele la wenye kuoa au kuolewa. Itakutokea vile kwa sababu wachuuzi wako walikuwa wenye uwezo mukubwa katika dunia, nawe umewadanganya watu wote kwa njia ya vitendo vyako vya uchawi.”


Kwa maana Mungu ametia ndani yao nia ya kuwasukuma kutimiza shabaha yake nao wapate kufikia shauri moja na kumupa yule nyama madaraka yao ya kifalme mpaka maneno ya Mungu yatimie.


Halafu mufalme akawaambia watumishi wake: ‘Mumufunge mutu huyu miguu na mikono na kumutupa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.’ ”


Kisha malaika mumoja mwenye uwezo akanyanyua jiwe linalokuwa kama jiwe kubwa la kusagia. Akalitupa katika bahari akisema: “Ni hivi muji mukubwa wa Babeli utakavyotupwa kwa nguvu, nao hautaonekana tena.


Na kule mutalia na kusaga meno, mutakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika Ufalme wa Mungu. Lakini ninyi mutakuwa mumetupwa inje!


Naye atamupiga vikali na atamwazibu sawa na watu wanafiki, akimuweka kwenye nafasi atakapolia na kusaga meno.


Alimwanga juu yao hasira yake kali, kasirani, chuki na taabu, na kuwashushia kundi la wamalaika waangamizaji.


“Hapa inafaa kuwa na akili na hekima. Vile vichwa saba ni milima saba, ambavyo yule mwanamuke anaikaa juu yake. Vile vichwa ni vilevile wafalme saba.


Na halafu watawatupa watu wabaya ndani ya furu la moto; na mule watalia na kusaga meno.”


Nao watawatupa ndani ya furu la moto, na mule watalia na kusaga meno.


Halafu akalalamika kwa sauti kubwa, akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa ule muji mukubwa Babeli! Sasa umekuwa makao ya mashetani ya kila namna, ya pepo wachafu, na makimbilio ya ndege wote wachafu na wenye kuchukiza.


Wakaaji wa dunia watafurahi kwa ajili ya kifo chao na kushangilia. Watatumiana zawadi, kwa maana manabii hawa wawili waliwasumbua sana wakaaji wa dunia.


Maiti zao zitabaki katika barabara ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa fumbo Sodoma au Misri. Ni ndani ya muji ule Bwana wao alitundikwa juu ya musalaba.


Lakini uache kiwanja kinachokuwa inje ya hekalu, usikipime kwa maana kimetolewa kwa watu wa mataifa mengine watakaokanyaga muji mutakatifu kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.


Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.


Kisha malaika wa ine akapiga baragumu. Sehemu moja ya tatu ya jua ikaharibishwa pamoja na sehemu moja ya tatu ya mwezi na ya nyota. Sehemu zile tatu zikaingiwa na giza. Hivi hakukuwa mwangaza kwa muda wa sehemu moja ya tatu ya saa za muchana na sehemu moja ya tatu ya saa za usiku vilevile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite