Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 16:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha nikasikia sauti kubwa ikitoka katika hekalu ikiwaambia wale wamalaika saba: “Mwende kumwanga vile vikombe saba vya kasirani ya Mungu juu ya dunia!”

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 16:1
17 Referans Kwoze  

Kwa hiyo muningojee mimi Yawe, ngoja siku nitakaposimama kutoa mashitaki. Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme, kuyamwangia kasirani yangu, na ukali wa hasira yangu. Dunia yote itateketezwa kwa moto wa kasirani yangu.


Kisha nikaona tena katika mbingu kitambulisho kingine kikubwa na cha kushangaza sana. Kulikuwa wamalaika saba wanaoshika mapigo saba. Mapigo haya ndiyo yaliyokuwa ya mwisho, kwa maana ni yale Mungu atakayotumia kwa kutimiza kasirani yake.


Umwange hasira yako juu ya mataifa yasiyokuabudu, na juu ya watu ambao hawakutambui. Maana, wamewaua wazao wa Yakobo; wamewaua na kuwaangamiza kabisa, na inchi yao wameiacha mabomoko.


Malaika wa saba akamwanga kikombe chake katika anga. Halafu sauti kubwa ikasikilika kutoka katika hekalu kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa ni mwisho!”


Uyamwangie mataifa yasiyokujua hasira yako, ndizo, tawala zote zisizoheshimu jina lako.


Mungu akamwambia yule mutu aliyevaa nguo ya kitani: Kwenda katikati ya magurudumu yanayokuwa chini ya makerubi, ujaze mikono yako na makaa ya moto unaokuwa katikati yao na kuyasambaza juu ya muji. Nikamwona akienda.


Kisha kukatokea malaika mwingine mwenye uwezo wa kuamuru moto, akatoka kwenye mazabahu, akamwambia kwa sauti kubwa yule aliyekuwa na kisu kikali cha kuvuna: “Nyoosha kisu chako, ukate matunda ya mizabibu yanayokuwa katika dunia kwa maana zabibu zimekomaa.”


Malaika mwingine akatoka katika hekalu, akalalamika kwa sauti kubwa akimwambia yule aliyeikaa juu ya wingu: “Nyoosha kisu chako, uanze kuvuna, kwa maana dunia iko tayari kwa kuvunwa, nayo saa ya mavuno imetimia!”


Sasa, uende kushambulia na kuangamiza vitu vyote wanavyokuwa navyo. Usiwaache wazima, lakini uwaue wote: wanaume kwa wanawake, watoto wachanga na wenye kunyonya, ngombe, kondoo, ngamia na punda.’ ”


Yawe alipokutuma alikuambia: ‘Kwenda uwaangamize kabisa wale Waamaleki wenye zambi, upigane nao mpaka umewaua wote!’


Kwa hiyo nimewamwangia kasirani yangu na kwa moto wa hasira yangu nimewateketeza kulingana na matendo yao. –Ndivyo anavyosema Bwana wetu Yawe.


Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite