Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 15:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha nikaona tena katika mbingu kitambulisho kingine kikubwa na cha kushangaza sana. Kulikuwa wamalaika saba wanaoshika mapigo saba. Mapigo haya ndiyo yaliyokuwa ya mwisho, kwa maana ni yale Mungu atakayotumia kwa kutimiza kasirani yake.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 15:1
21 Referans Kwoze  

Kama mukiendelea kunipinga na kukataa kunisikiliza, nitazidisha tena azabu yenu mara saba kadiri ya wingi wa zambi zenu.


Kisha mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe vilivyojaa mapigo saba ya mwisho, akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha bibi arusi, muke wa Mwana-Kondoo.”


Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga mukali kwa kushinda mataifa. Naye atatawala kwa fimbo ya chuma na kukamua zabibu ndani ya kikamulio cha divai kinachojaa kasirani kali ya Mungu Mwenye Uwezo.


Kisha nikasikia sauti kubwa ikitoka katika hekalu ikiwaambia wale wamalaika saba: “Mwende kumwanga vile vikombe saba vya kasirani ya Mungu juu ya dunia!”


Yule malaika akanyoosha kisu chake juu ya dunia, akachuma mizabibu ya dunia, akaitupa katika kikamulio kikubwa cha zabibu chenye kujaa kasirani ya Mungu.


naye vilevile atakunywa divai kali ya hasira ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchangwa na maji na kumimiwa ndani ya kikombe chenye kujaa kasirani yake! Na watu kama wale, watateswa ndani ya moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto mbele ya wamalaika watakatifu na mbele ya Mwana- Kondoo.


Ninatoa amri katika ufalme wangu kwamba watu wote wanapaswa kumwogopa na kumuheshimu Mungu wa Danieli. Yeye ni Mungu Mwenye Uzima, anayeishi milele; ufalme wake hauwezi kuangamizwa hata kidogo, utawala wake hauna mwisho.


Hasara ya pili imepita, na hasara ya tatu haitakawia kutokea!


Akalalamika kwa sauti kubwa kama simba anayenguruma. Na alipokwisha kulalamika, kukasikilika mulio wa ngurumo saba ya radi.


Wale wamalaika saba waliokuwa na baragumu saba wakajitayarisha kwa kuzipiga.


Kisha nikaangalia tena, nami nikasikia tai mumoja akiruka juu sana katika anga akisema hivi kwa sauti kubwa: “Ole! Ole! Ole kwa wakaaji wa dunia, kutakaposikilika mulio wa zile baragumu zingine ambazo wamalaika watatu wanatayarisha kupiga!”


Kisha nikaona wamalaika saba wakisimama mbele ya Mungu, nao wakapewa baragumu saba.


Watu waliobaki bila kuuawa na yale mapigo hawakuachana na sanamu walizojitengenezea wao wenyewe. Hawakuacha kuabudu pepo, sanamu za zahabu, za feza, za shaba, za mawe na za miti zisizoweza kuona, wala kusikia, wala kutembea.


Halafu mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe saba akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha namna gani yule kahaba mukubwa atakavyohukumiwa, ndio ule muji uliojengwa katikati ya mito mingi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite