Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliimba wimbo mupya mbele ya kile kiti cha kifalme na mbele ya vile viumbe vine vya ajabu na ya wale wazee. Hakuna mutu aliyeweza kujifunza wimbo ule, isipokuwa wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliokombolewa katika dunia.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 14:3
17 Referans Kwoze  

Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Kisha nikaangalia, nikaona Mwana-Kondoo akisimama juu ya mulima Sayuni. Naye alikuwa pamoja na watu elfu mia moja makumi ine na ine, na juu ya paji za nyuso za watu wale kulikuwa kumeandikwa jina lake na jina la Baba yake.


Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


Haleluia! Mumwimbie Yawe wimbo mupya; mumusifu katika kusanyiko la waaminifu!


Zaburi. Mumwimbie Yawe wimbo mupya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu! Nguvu yake kubwa, mukono wake mutakatifu umemupatia ushindi.


Aliniondoa katika shimo la hatari, alinitoa katika matope mengi, akanisimamisha salama juu ya mulima, na kuziimarisha hatua zangu.


Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mupya; nitakupigia kinubi cha nyuzi kumi,


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Mumwimbie Yawe, ninyi ulimwengu wote!


Mumwimbie wimbo mupya; mupige kinubi vizuri na kushangilia.


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Hivi, mahubiri ya kufa kwa Kristo juu ya musalaba yanahesabiwa kuwa upumbafu kwa wale wanaopotea. Lakini kwa sisi tunaookolewa ni uwezo wa Mungu.


Nikasikia hesabu ya watu waliopigwa chapa ya muhuri wa Mungu ilikuwa: elfu mia moja na makumi ine na ine kutoka makabila yote ya Waisraeli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite