Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 14:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikinguruma kama uvumi wa maporomoko ya maji mengi na kama ngurumo kubwa ya radi. Sauti ile ilisikilika kama vile sauti ya wapiga vinubi wakati wanapopiga vinubi vyao.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 14:2
29 Referans Kwoze  

Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.


Miguu yake ilingaa kama shaba iliyosafishwa vizuri sana katika furu ya moto, na sauti yake ilinguruma kama maporomoko ya maji mengi.


Tena nikaona kitu kinachofanana na bahari ya kioo, iliyochanganyika na moto. Nikaona vilevile wale walioshinda yule nyama wa ajabu pamoja na sanamu yake na tarakimu zinazolingana na herufi za jina lake. Watu wale walikuwa wakisimama juu ya ile bahari ya kioo wakishika vinubi walivyopewa na Mungu.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea upande wa mashariki. Pamoja nao kulikuwa mushindo wa kuja kwake kama mushindo wa maji mengi, inchi ilingaa kwa utukufu wake.


Mumusifu Yawe kwa zeze; mumwimbie kwa kinubi cha nyuzi kumi.


Daudi na watu wote wa Israeli, walikuwa wanaimba nyimbo na kucheza kwa nguvu zao zote, mbele ya Yawe. Walipiga ala za muziki zilizotengenezwa na muti wa muvinje: vinubi, vinanda, matari, kayamba na matoazi.


Basi, siku ya tatu asubui, kukatokea ngurumo na umeme na wingu zito juu ya mulima. Kukasikilika vilevile sauti kubwa ya baragumu ambayo iliwatetemesha watu wote katika kambi.


Sauti ya wapiga vinubi na ya wapiga vinanda, ya wapiga filimbi na ya baragumu, haitasikilika ndani yako tena. Fundi wa kazi yoyote hataonekana ndani yako tena hata kidogo wala kelele la jiwe la kusagia halitasikilika.


Manabii hao wawili wakasikia sauti kubwa toka mbinguni ikiwaambia: “Mupande huku!” Wakapanda mbinguni wakizungukwa na wingu, wale waadui zao wakiwa wakiwaangalia.


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa kwanza kati ya ile mihuri saba, nikasikia kimoja kati ya vile viumbe vya ajabu kikisema hivi kwa sauti kama ya ngurumo ya radi: “Kuja!”


Siku moja ya kumwabudu Bwana, nikashikwa na Roho wa Mungu, nikasikia sauti kubwa, inayolia kama baragumu,


Yawe ana mamlaka juu mbinguni, ana nguvu kuliko mulio wa bahari, ana nguvu kuliko mawimbi ya maji.


Ni vizuri kutangaza wema wako asubui, na uaminifu wako kwa wakati wa usiku,


Moyo wangu ni tayari, ee Mungu, moyo wangu ni tayari; nitaimba na kukushangilia!


Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.


Yawe atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana wetu Yawe atapiga baragumu; atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.


Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.


Mulisifu jina lake mukicheza, mumwimbie kwa ngoma na zeze.


Mumusifu Yawe kwa shangwe, mumusifu kwa sauti tamu za zeze.


Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,


Mumwimbie Yawe nyimbo za shukrani, mumupigie Mungu wetu kinubi!


Hapo, ee Mungu, nitakwenda kwenye mazabahu yako; nitakuja kwako, ee Mungu, wewe furaha yangu kubwa. Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu.


Hata nikiwa na uwezo wa kusema luga za watu na za wamalaika, lakini kama sina upendo, masemi yangu ni bure kama vile kelele la kengele au matoazi.


Walipofika Yerusalema, walikwenda moja kwa moja mpaka kwenye nyumba ya Yawe, wakipiga vinanda, vinubi na baragumu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite