Ufunuo 13:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 Yule nyama akapewa uwezo wa kusema maneno ya kiburi ya kumutukana Mungu. Naye akapewa mamlaka ya kufanya kazi yake kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.
Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.
Nilipokuwa ninaziangalia hizo pembe, niliona pembe ingine ndogo ikiota katikati ya zile kumi, nayo ikaongoa pembe tatu kati ya hizo za kwanza. Pembe ile ilikuwa na macho ya kimutu na kinywa kilichosema maneno ya kujivuna.
Na yule mwanamuke akakimbilia katika jangwa kwenye nafasi Mungu aliyomutayarishia kusudi apate kulishwa kule kwa muda wa siku elfu moja mia mbili makumi sita.
Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.
Kutokana na maneno ya kujivuna yaliyokuwa yanasemwa na ile pembe, nikaendelea kuangalia. Nikaona yule nyama wa ine akiuawa, mwili wake ukaharibiwa na kutolewa uchomwe kwa moto.
Lakini yule mwanamuke akapewa mabawa mawili yanayokuwa kama ya tai, kusudi apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye nafasi aliyotengenezewa, mbali na yule nyoka. Na kule apate kukulishwa kwa muda wa miaka mitatu na nusu.
Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.
Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.
Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watu wa Mungu na kuwashinda. Akapewa hata mamlaka ya kutawala watu wote, wa kila kabila, kila jamaa, kila luga na kila taifa.
Yule mutakatifu wa kwanza akamujibu: Kwa muda wa nyakati za magaribi na asubui elfu mbili mia tatu. Kisha hekalu la Mungu litapata tena hali yake kamili.
Musikubali kudanganywa na mutu yeyote kwa namna yoyote. Kwa maana Siku ile haitatimia mpaka kwanza ule uasi mukubwa utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa.