Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 13:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Na yule nyama akawalazimisha watu wote, wadogo na wakubwa, watajiri na wamasikini, wanaokuwa huru na watumwa, wapigwe chapa juu ya mikono yao ya kuume na juu ya paji za nyuso zao.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 13:16
26 Referans Kwoze  

Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


“Musiharibu dunia, wala bahari, wala miti mpaka tutakapokwisha kutia chapa ya muhuri juu ya paji ya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”


akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.


Hivi mutakula nyama za miili ya wafalme, za majemadari, za watu wenye uwezo, nyama za farasi pamoja na za watu wanaopanda juu yao na nyama za watu wote wanaokuwa huru na za watumwa, wakubwa kama vile wadogo.”


Muyafunge katika mikono yenu na kuyavaa katika paji za nyuso zenu kama vile ukumbusho.


“Muweke maneno yangu haya ndani ya mioyo yenu na roho zenu. Muyafungie katika mikono yenu kama vile kitambulisho na kuyavaa katika paji la uso.


Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.


Kisha sauti ikasikilika toka kwenye kiti cha kifalme ikasema: “Mumusifu Mungu wetu ninyi watumishi wake wote, ninyi wote munaomuheshimu, wakubwa na wadogo!”


Nikaona wale waliokufa, wakubwa na wadogo wakisimama mbele ya kile kiti cha kifalme. Vitabu vikafunguliwa na kitabu kingine kikafunguliwa ndicho kitabu cha uzima. Wale waliokufa wakahukumiwa kufuatana na matendo yao sawa vile ilivyoandikwa katika vitabu.


Wafalme wa dunia, wakubwa, wakubwa wa waaskari, watajiri, wenye uwezo, na watu wengine wote, watumwa au wenye kuwa huru wakajificha katika mapango na katikati ya mawe ya milima.


Lakini kwa ulinzi wa Mungu ningali muzima hata leo. Nami ninatoa ushuhuda kwa wadogo na wakubwa, wala sisemi maneno mengine yanayokuwa mbali na yale manabii na Musa waliyosema kwamba yatatokea.


atawabariki wote wanaomwabudu, atawabariki wakubwa kama vile wadogo.


Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.


Tena nikaona kitu kinachofanana na bahari ya kioo, iliyochanganyika na moto. Nikaona vilevile wale walioshinda yule nyama wa ajabu pamoja na sanamu yake na tarakimu zinazolingana na herufi za jina lake. Watu wale walikuwa wakisimama juu ya ile bahari ya kioo wakishika vinubi walivyopewa na Mungu.


Watu wa mataifa mengine walikasirika, lakini kasirani yako imetokea. Sasa ni wakati wa kuhukumu waliokufa, nao wakati wa kuwapa waliokutumikia zawadi, ndio manabii wako, na wote wanaoheshimu jina lako, wakubwa na wadogo. Ni wakati wa kuangamiza wale wanaoharibu dunia!”


Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.


Mukumbuke kwamba Bwana atalipa kila mutu sawa na matendo yake mema, akiwa huru au mutumwa.


Basi sasa, mutu asinisumbue tena kwa maana niko na makovu juu ya mwili wangu niliyopata kwa ajili ya Yesu.


Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Vilevile sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mumoja kusudi tukuwe mwili mumoja na sisi wote tumekunyweshwa Roho mumoja.


Musikie jambo hili, enyi watu wote! Mutege masikio, enyi wakaaji wote wa dunia.


na kwamba yeyote asiyemutafuta Yawe, Mungu wa Israeli, akuwe kijana au muzee, mwanaume au mwanamuke, sharti auawe.


Watu wale wanapinga ukweli kama vile Yane na Yambure walivyopingana na Musa. Akili ya watu hao imepotoka, nayo imani yao imegeuka bure.


Na mutu akimwuliza mumoja wao: “Vidonda hivi unavyokuwa navyo kwenye mikono yako vimetoka wapi?” Yeye atajibu: “Vidonda hivi nilivipata katika nyumba ya warafiki zangu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite