Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 13:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha nikaona nyama mumoja wa ajabu akitokea ndani ya bahari. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. Na juu ya kila pembe lake kulikuwa taji, na juu ya vichwa vile kulikuwa kumeandikwa jina la kumutukana Mungu.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 13:1
21 Referans Kwoze  

Kisha kukaonekana kitambulisho kingine mbinguni. Kulikuwa nyoka mukubwa mwekundu mwenye vichwa saba na pembe kumi. Juu ya kila kichwa kulikuwa taji saba.


Nikashikwa na Roho wa Mungu, na malaika akanipeleka katika jangwa. Kule nikaona mwanamuke aliyekuwa akiikaa juu ya nyama mumoja wa ajabu mwekundu aliyeandikwa juu yake majina ya kumutukana Mungu. Nyama yule alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.


Wakati watakapomaliza kutoa huo ushuhuda wa Mungu, yule nyama wa ajabu anayetoka katika kuzimu atapigana vita nao, naye atawashinda na kuwaua.


Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.


Zile pembe kumi ulizoona na yule nyama wa ajabu watamuchukia yule kahaba. Watamunyanganya vyote anavyokuwa navyo na kumwacha uchi. Nao watakula nyama ya mwili wake na kuteketeza mabaki yake kwa moto.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Tena nikaona kitu kinachofanana na bahari ya kioo, iliyochanganyika na moto. Nikaona vilevile wale walioshinda yule nyama wa ajabu pamoja na sanamu yake na tarakimu zinazolingana na herufi za jina lake. Watu wale walikuwa wakisimama juu ya ile bahari ya kioo wakishika vinubi walivyopewa na Mungu.


Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina lenye fumbo: “Muji mukubwa Babeli, mama ya washerati na machukizo ya dunia.”


Kisha nikaona nyama wa pili wa ajabu akitokea ndani ya udongo. Alikuwa na pembe mbili zinazokuwa kama za mwana-kondoo naye alikuwa akisema kama nyoka mukubwa.


Akawadanganya wakaaji wa dunia kwa njia ya vitambulisho alivyowezeshwa kuonyesha mbele ya yule nyama mukubwa wa kwanza. Aliwaambia watu wa dunia watengeneze sanamu kwa heshima ya yule nyama aliyeumizwa kwa upanga, lakini aliendelea kuishi.


Kisha yule nyama mukubwa wa pili akapewa uwezo wa kupuliza pumzi ya uzima ndani ya sanamu ya yule nyama mukubwa wa kwanza kusudi sanamu ile ipate kusema na kuweza kuua watu wasioiabudu.


Halafu nikaona pepo wachafu watatu wanaofanana na vyura wakitoka ndani ya kinywa cha yule nyoka mukubwa, na ndani ya kinywa cha yule nyama wa ajabu na cha yule nabii wa uongo.


Nikaona yule nyama wa ajabu pamoja na wafalme wa dunia na makundi yao ya waaskari wamekusanyika pamoja kupigana vita na yule anayepanda juu ya farasi na kundi la waaskari wake.


Uliona vilevile kwamba vikanyagio na vidole vya sanamu hiyo vilikuwa nusu udongo wa mufinyanzi na nusu chuma. Hii ina maana kwamba ufalme huo utagawanyika; lakini ndani yake kutakuwa nguvu za chuma kwa sababu kulikuwa chuma kilichochanganyikana na udongo wa mufinyanzi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite