Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 12:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 lakini akashindwa na haikuwezekana tena kwake kukaa mbinguni pamoja na wamalaika zake.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 12:8
18 Referans Kwoze  

Bado kidogo, mwovu atatoweka; utamutafuta pale alipokuwa, wala hautamwona.


Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.


Watapigana nawe, lakini hawatashinda, kwa sababu mimi niko pamoja nawe kwa kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mukumbuke vilevile wamalaika wale waliokosa kulinda vema cheo chao, lakini wakaacha makao yao: Mungu akawaweka katika nafasi ya giza, wakifungwa minyororo ya milele kwa kungojea Siku ile ya hukumu.


kusudi atiwe katika kazi hii ya kuwa mutume kwenye nafasi Yuda aliyoacha na kwenda pahali pake mwenyewe.”


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu, lakini hawakunishinda.


Uniangalie na kunijibu, ee Yawe, Mungu wangu. Uyaangazie macho yangu, nisipatwe na usingizi wa kifo.


Aliyemwona, hatamwona tena, wala pale alipoishi hapatatambuliwa tena.


Lakini likiangamizwa kutoka makao yake, hayo yatalikana yakisema: “Sijakuona bado.”


Anayeondoka harudi tena kwa jamaa yake, na pale alipokuwa anaishi, wanamusahau mara moja.


Halafu kukatokea vita katika mbingu. Mikaeli na wamalaika zake wakapigana na yule nyoka mukubwa. Naye yule nyoka akapigana nao pamoja na wamalaika zake,


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite