Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kisha kukaonekana kitambulisho kingine mbinguni. Kulikuwa nyoka mukubwa mwekundu mwenye vichwa saba na pembe kumi. Juu ya kila kichwa kulikuwa taji saba.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 12:3
27 Referans Kwoze  

“Zile pembe kumi ulizoona ni wafalme kumi, ambao hawajaanza bado kutawala, lakini watapewa mamlaka ya kutawala kama wafalme kwa muda wa saa moja pamoja na yule nyama.


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Zile pembe kumi ulizoona na yule nyama wa ajabu watamuchukia yule kahaba. Watamunyanganya vyote anavyokuwa navyo na kumwacha uchi. Nao watakula nyama ya mwili wake na kuteketeza mabaki yake kwa moto.


Halafu yule malaika akaniuliza: “Kwa nini unashangaa? Nitakuambia maana ya fumbo la mwanamuke yule na ya yule nyama anayemubeba, na anayekuwa na vichwa saba na pembe kumi.


Zile pembe kumi ni wafalme kumi watakaotokana na ufalme huo. Halafu watafuatwa na mufalme mwingine ambaye atakuwa tofauti na wale waliomutangulia, na atawaangusha wafalme watatu.


Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.


Akamukamata yule nyoka mukubwa, ndiye yule nyoka wa zamani, anayeitwa “Mwovu” au “Shetani” na kumufunga kwa muda wa miaka elfu moja.


Mukia wake ulikokota sehemu moja ya tatu ya nyota za mbingu na kuzitupa katika dunia. Yule nyoka akasimama mbele ya yule mwanamuke aliyekuwa tayari kuzaa, kusudi amumeze mutoto wakati atakapozaliwa.


Kisha kukaonekana kitambulisho kikubwa mbinguni. Kulikuwa mwanamuke aliyekuwa amefunikwa na jua, na mwezi chini kwenye miguu yake. Na juu ya kichwa kulikuwa taji lenye nyota kumi na mbili.


Halafu nikaona pepo wachafu watatu wanaofanana na vyura wakitoka ndani ya kinywa cha yule nyoka mukubwa, na ndani ya kinywa cha yule nyama wa ajabu na cha yule nabii wa uongo.


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Siku hiyo, Yawe atakamata upanga wake mukubwa, mukali na imara, na kuiazibu Leviatani, ile nyoka inayoruka na kuzongazonga. Yawe ataua nyoka mukubwa anayeishi katika bahari.


Macho yake yalimetameta kama ndimi za moto, na juu ya kichwa chake kulikuwa taji nyingi. Alikuwa na jina lililoandikwa juu yake, wala hakuna mutu aliyejua, isipokuwa yeye mwenyewe tu.


Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


Wale wanaoongoza watu hawa wamewapotosha, na hao wanaoongozwa nao wamepotoka.


Kama ulivyoona, vidole vyake vya miguu vilikuwa nusu chuma na nusu udongo wa mufinyanzi, na hii ina maana kwamba ufalme ule utakuwa na sehemu moja yenye nguvu na sehemu ingine yenye uzaifu.


Halafu kukatokea vita katika mbingu. Mikaeli na wamalaika zake wakapigana na yule nyoka mukubwa. Naye yule nyoka akapigana nao pamoja na wamalaika zake,


Na wakati yule nyoka alipotambua kwamba ametupwa katika dunia, akaanza kumufuatilia yule mwanamuke aliyezaa mutoto mwanaume.


Kisha nikaona nyama mumoja wa ajabu akitokea ndani ya bahari. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. Na juu ya kila pembe lake kulikuwa taji, na juu ya vichwa vile kulikuwa kumeandikwa jina la kumutukana Mungu.


Yule nyama niliyemwona alifanana na chui. Miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Yule nyoka mukubwa akamupa uwezo wake pamoja na kiti chake cha kifalme na mamlaka makubwa.


Nao wakaanza kumwabudu yule nyoka kwa sababu alimupa yule nyama uwezo wake. Vilevile wakamwabudu yule nyama, wakisema: “Ni nani anayefanana na nyama huyu? Ni nani anayeweza kupigana vita naye?”


Kisha nikaona tena katika mbingu kitambulisho kingine kikubwa na cha kushangaza sana. Kulikuwa wamalaika saba wanaoshika mapigo saba. Mapigo haya ndiyo yaliyokuwa ya mwisho, kwa maana ni yale Mungu atakayotumia kwa kutimiza kasirani yake.


Uliona vilevile kwamba vikanyagio na vidole vya sanamu hiyo vilikuwa nusu udongo wa mufinyanzi na nusu chuma. Hii ina maana kwamba ufalme huo utagawanyika; lakini ndani yake kutakuwa nguvu za chuma kwa sababu kulikuwa chuma kilichochanganyikana na udongo wa mufinyanzi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite