Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 12:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 12:10
24 Referans Kwoze  

“Simoni, Simoni! Sikiliza: Shetani ameachiliwa wakati wa kuwajaribu na kuwatenga kabisa.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Lakini sasa, unyooshe mukono wako uguse mali yake. Utaona namna atakutukana waziwazi!”


Shetani akamujibu Yawe: “Yobu anamwogopa Yawe kwa bure?


Na yule atakayeshinda na kuendelea kufuata mapenzi yangu mpaka mwisho, nitamupa mamlaka ya kutawala mataifa.


Lakini akanijibu: “Neema yangu inakutoshelea, kwa maana uwezo wangu unatimizwa katika uzaifu.” Basi tafazali nijivunie sana uzaifu wangu kusudi nijazwe na uwezo wa Kristo.


Yesu akawaambia: “Munapoomba, museme: ‘Baba! Jina lako litukuzwe; Ufalme wako ukuje.


Yesu akamujibu: “Wewe umesema. Lakini zaidi ya hiyo, ninawaambia ninyi kwamba mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka karibu na Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”


Ufalme wako ukuje; mapenzi yako yafanyike katika dunia kama inavyokuwa mbinguni.


Ulimwengu wote utakumbuka na kumurudilia Yawe; jamaa zote za mataifa zitamwabudu.


Lakini sasa, unyooshe mukono wako umuguse mwili wake. Utaona namna atakutukana waziwazi.”


Vilevile uwaambie wanawake wazee wakuwe na mwenendo unaostahili kwa watu watakatifu. Hawapaswi kuwa wasingiziaji, wala wasikuwe watumwa wa pombe, lakini wakuwe wenye kutoa mafundisho mazuri.


Mishale yako ni mikali, inapenya mioyo ya waadui za mufalme; nayo mataifa yanaanguka chini yako.


Nao walilalamika hivi kwa sauti kubwa: “Wokovu wetu unatoka kwa Mungu wetu anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo!”


Mukuwe waangalifu na mukeshe, kwa maana adui yenu Shetani anazungukazunguka kama simba anayenguruma akitafuta yule atakayerarua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite