Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 11:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Maiti zao zitabaki katika barabara ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa fumbo Sodoma au Misri. Ni ndani ya muji ule Bwana wao alitundikwa juu ya musalaba.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 11:8
40 Referans Kwoze  

Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


Watasimama kwa mbali kwa ajili ya kuogopa yale mateso yake, wakisema: “Ole, ole kwako ewe muji Babeli, muji mukubwa na wenye uwezo! Kwa saa moja tu azabu yako imetimia!”


Kisha malaika mumoja mwenye uwezo akanyanyua jiwe linalokuwa kama jiwe kubwa la kusagia. Akalitupa katika bahari akisema: “Ni hivi muji mukubwa wa Babeli utakavyotupwa kwa nguvu, nao hautaonekana tena.


Kwa sababu hii Yesu vilevile aliuawa mbali na muji kusudi awatakase watu wake kwa njia ya damu yake mwenyewe.


Walilalamika walipoona moshi wa moto uliouteketeza ukipanda juu wakisema: “Muji gani ungeweza kulinganishwa na muji huu mukubwa!”


Nao watu wa kila jamaa, wa kila kabila, wa kila luga na wa kila taifa wataangalia maiti hizo kwa muda wa siku tatu na nusu, wala hawatakubali zizikwe.


Mukumbuke vilevile watu wa Sodoma na Gomora na wa miji iliyokuwa kandokando wanaokuwa sawasawa na wamalaika hawa. Walifanya uasherati na mambo ya kimwili yasiyokuwa ya kawaida ya asili. Watu hawa wanapokea hukumu ya moto wa milele kuwa mufano wazi kwa watu wote.


Vilevile Mungu alihukumu muji wa Sodoma na Gomora na kuiteketeza kwa moto. Kwa njia hiyo, alionyesha mufano wa mambo yatakayotokea kwa watu waovu.


Kweli ninawaambia: kwa Siku ya hukumu, watu wa muji ule wataazibiwa vikali zaidi kuliko watu wa muji wa Sodoma na wa Gomora.


Niliwaangusha wamoja kati yenu kwa maangamizi kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Wale waliobaki kati yenu, walikuwa kama kijiti kilichookolewa katika moto. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitaukomesha uasherati na uzinzi wako ulioufanya tangu ulipokuwa kule Misri. Hautaziangalia sanamu zozote tena wala kuifikiria tena inchi ya Misri.


Hata hivyo, akazidisha uzinzi wake akifanya kama wakati wa ujana wake alipofanya uzinzi kule Misri.


Aliendelea na uzinzi wake aliouanza kule Misri wakati huo wa ujana wake, wanaume walivunja ubikira wake na kuzitimiza tamaa zao kwake.


Katika ujana wao walipokuwa wanakaa kule Misri, wakakubali maziba yao kupapaswa, wakapoteza ubikira wao, wakafanya uzinzi.


Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Halafu Yawe akateremusha moto mukali wa kiberiti kutoka mbinguni juu ya Sodoma na Gomora,


Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


Halafu akalalamika kwa sauti kubwa, akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa ule muji mukubwa Babeli! Sasa umekuwa makao ya mashetani ya kila namna, ya pepo wachafu, na makimbilio ya ndege wote wachafu na wenye kuchukiza.


Na ule muji mukubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa yote ikabomoka. Mungu hakusahau muji mukubwa Babeli, akaukunywesha kikombe kinachokuwa na divai ya kasirani yake kali.


Malaika wa pili akafuata yule wa kwanza akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa, ule muji mukubwa Babeli. Umewakunywesha mataifa yote divai yake kali, ukiwalewesha na maovu ya uasherati wake.”


Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.


kisha wakianguka, haiwezekani kuwarudisha hata wapate kugeuka mara ingine toka katika matendo yao mabaya. Kwa sababu wamemutundika wao wenyewe Mwana wa Mungu mara ya pili na kumupatisha haya mbele ya watu.


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Wao wakamurudisha Uria kutoka Misri, wakamupeleka kwa mufalme Yoyakimu. Mufalme akamwua kwa upanga na maiti yake ikatupwa katika kaburi.


Muji Babeli umeazibiwa kwa sababu ndani yake kumeonekana damu ya manabii na ya watu wa Mungu pamoja na damu ya watu wote waliouawa katika dunia.


Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina lenye fumbo: “Muji mukubwa Babeli, mama ya washerati na machukizo ya dunia.”


Halafu mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe saba akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha namna gani yule kahaba mukubwa atakavyohukumiwa, ndio ule muji uliojengwa katikati ya mito mingi.


Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.


Dada yako mukubwa ni Samaria, aliyekaa upande wako wa kaskazini pamoja na wabinti zake. Dada yako mudogo ni Sodoma, aliyekaa upande wako wa kusini pamoja na wabinti zake.


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Zile zabibu zikakamuliwa mbali na muji, damu ikatiririka toka ndani ya kile kikamulio mpaka ikafika kwenye umbali wa kilometre yapata mia tatu. Nao urefu kwenda chini wa ile damu ulikuwa yapata metre moja na nusu.


Yule mwanamuke uliyemwona, ni ule muji mukubwa unaotawala wafalme wa dunia.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite