Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha wakanipa fimbo ya kupima urefu na kuniambia: “Simama upime hekalu la Mungu pamoja na mazabahu na kuwahesabu watu wanaoabudu ndani yake.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 11:1
15 Referans Kwoze  

Malaika yule aliyekuwa akisema nami alikuwa na fimbo ya kupima ya zahabu kusudi apate kupima muji ule, milango yake na ukuta unaouzunguka.


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”


Kutoka Haseroti, wakapiga kambi yao huko Ritima.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Kisha wakaniambia: “Imekupasa kutoa unabii tena kwa jamaa, kwa mataifa, kwa watu wa kila luga na kwa wafalme wengi.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite