Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 10:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kisha wakaniambia: “Imekupasa kutoa unabii tena kwa jamaa, kwa mataifa, kwa watu wa kila luga na kwa wafalme wengi.”

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 10:11
13 Referans Kwoze  

Naye akaniambia: Toa unabii juu ya mifupa hii. Uiambie hivi: Enyi mifupa yenye kukauka, musikilize neno la Yawe.


Yule malaika akaniambia tena: “Yale maji uliyoona pale yule kahaba anapoikaa, ni watu wa kila taifa, kila jamaa na kila luga.


Kisha nikaona malaika mwingine akiruka juu sana katika mbingu akiwa na Habari Njema ya milele ya kupasha kwa wakaaji wa dunia, kwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila luga na kila jamaa.


Nao watu wa kila jamaa, wa kila kabila, wa kila luga na wa kila taifa wataangalia maiti hizo kwa muda wa siku tatu na nusu, wala hawatakubali zizikwe.


Halafu, Yawe akaniambia: Ewe mwanadamu, kwa ajili yangu toa unabii kwa upepo, uuambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe upepo kuja toka pande zote ine na kuipulizia miili hii iliyokufa kusudi ipate kuishi.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Basi nikatwaa kitabu kile kidogo toka katika mukono wake, nikakikula. Kikakuwa kitamu kama asali ndani ya kinywa changu, lakini wakati nilipokimeza, nikasikia uchungu ndani ya tumbo langu.


Kisha wakanipa fimbo ya kupima urefu na kuniambia: “Simama upime hekalu la Mungu pamoja na mazabahu na kuwahesabu watu wanaoabudu ndani yake.


Watano kati yao wamekwisha kuangushwa chini, mumoja angali anatawala na mwingine hajafika bado; naye atakapofika, atabaki kwa muda mufupi tu.


“Zile pembe kumi ulizoona ni wafalme kumi, ambao hawajaanza bado kutawala, lakini watapewa mamlaka ya kutawala kama wafalme kwa muda wa saa moja pamoja na yule nyama.


Nitaleta juu ya inchi hiyo mambo yote niliyosema juu yake na yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki ambayo Yeremia alitabiri juu ya mataifa yote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite