Kisha nikaona malaika mwingine akiruka juu sana katika mbingu akiwa na Habari Njema ya milele ya kupasha kwa wakaaji wa dunia, kwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila luga na kila jamaa.
Halafu, Yawe akaniambia: Ewe mwanadamu, kwa ajili yangu toa unabii kwa upepo, uuambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe upepo kuja toka pande zote ine na kuipulizia miili hii iliyokufa kusudi ipate kuishi.
Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.
Basi nikatwaa kitabu kile kidogo toka katika mukono wake, nikakikula. Kikakuwa kitamu kama asali ndani ya kinywa changu, lakini wakati nilipokimeza, nikasikia uchungu ndani ya tumbo langu.
“Zile pembe kumi ulizoona ni wafalme kumi, ambao hawajaanza bado kutawala, lakini watapewa mamlaka ya kutawala kama wafalme kwa muda wa saa moja pamoja na yule nyama.