Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Na katikati ya vile vinara saba, nikaona kiumbe kimoja kinachofanana na Mwana wa Mutu. Naye alikuwa amevaa kanzu ndefu inayofika hata kwenye miguu yake na mukaba wa zahabu katika kifua chake.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 1:13
15 Referans Kwoze  

Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake.


Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.


Na wale wamalaika saba walioshika mapigo saba wakatoka katika lile hekalu. Walikuwa wamevaa nguo zilizofumwa na nyuzi za pamba zenye kungaa na mikaba ya zahabu katika viuno vyao.


Niliangalia tena, nami nikaona wingu jeupe, na juu ya wingu lile kulikuwa kukiikaa kiumbe kimoja kinachofanana na Mwana wa Mutu. Juu ya kichwa chake kulikuwa taji la zahabu, naye alikuwa akishika kisu kikali cha kuvuna katika mukono wake.


Kisha akamuvalisha Haruni koti na kuifunga kwa mukaba, akamuvalisha kanzu, akamuvalisha kizibao na kukifunga kwenye kiuno chake kwa mukaba uliofumwa kwa ufundi.


Nilipokuwa nikiendelea kuangalia, nikaona viti vya kifalme viliwekwa hapo, kisha Muzee mumoja wa zamani sana akakuja, akaikaa. Alikuwa amevaa nguo nyeupe kama teluji; nywele zake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha kifalme kilikuwa ndimi za moto, na magurudumu ya kiti kile yalikuwa moto unaowaka.


Haki itakuwa kama mukaba wa kujifunga, uaminifu utakuwa kama mukaba kwenye kiuno chake.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Mukaba uliofumwa kwa ufundi juu yake kwa kuifunga ulikuwa kitu kimoja na kizibao hicho, na ulitengenezwa kwa vitu hivyohivyo: zahabu, sufu ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Efeso hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeshika nyota saba katika mukono wake wa kuume na anayetembea katikati ya vinara saba vya taa vya zahabu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite