Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi nikageuka kusudi nione yule aliyesema nami. Na wakati nilipogeuka nikaona vinara saba vya taa vilivyotengenezwa na zahabu.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 1:12
11 Referans Kwoze  

Akaniuliza: Unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kinara cha taa cha zahabu. Juu yake kuna bakuli la mafuta na taa saba, na kila moja ina pahali pa kutilia tambi saba.


Utatengeneza vilevile taa saba kwa ajili ya kinara kile na kuziweka juu yake kusudi ziangaze kwa mbele.


Hii ndiyo maana ya lile fumbo juu ya zile nyota saba ulizoona katika mukono wangu wa kuume, na vile vinara saba vya zahabu: zile nyota saba ni wamalaika wa makanisa saba na vile vinara saba ni yale makanisa saba.


Na katikati ya vile vinara saba, nikaona kiumbe kimoja kinachofanana na Mwana wa Mutu. Naye alikuwa amevaa kanzu ndefu inayofika hata kwenye miguu yake na mukaba wa zahabu katika kifua chake.


Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.


Akatengeneza taa zake saba, koleo zake na visahani vyake kwa zahabu safi.


Basi uandike mambo unayoona, na mambo yanayokuwa sasa na yale yatakayotokea nyuma.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Efeso hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeshika nyota saba katika mukono wake wa kuume na anayetembea katikati ya vinara saba vya taa vya zahabu.


Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite