Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Tito 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.

Gade chapit la Kopi




Tito 3:8
26 Referans Kwoze  

Inafaa watu wetu vilevile wajifunze kuzidi kutenda mema kusudi wapate kutoa musaada kwa ajili ya mahitaji ya kweli. Na hivi maisha yao yatakuwa yenye mafaa.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Anapaswa kushika Neno la kweli linalolingana na mafundisho yetu. Hivi ataweza kuwaonya watu kwa njia ya mafundisho ya kweli na kuwashinda wale wanaomupinga.


Uwakumbushe watu wajinyenyekeze mbele ya watawala na wakubwa. Wanapaswa kuwatii na kuwa tayari kwa kufanya kila tendo zuri.


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Neno hili ni la kuaminiwa nalo linastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja katika dunia kwa kuokoa wenye zambi. Na mimi ni wa kwanza mwenye zambi kati yao,


Lakini mutu asipotegemea matendo yake mwenyewe, naye akimwamini Mungu anayemuhesabia mwovu haki, basi imani yake inahesabiwa kuwa haki.


Halafu Yesu akasema hivi kwa sauti: “Anayeniamini haniamini mimi tu, lakini anamwamini vilevile yule aliyenituma.


“Kweli, kweli ninawaambia: anayesikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma, anapata uzima wa milele. Yeye hatahukumiwa, lakini ameponyoka lufu na kupata uzima.


Mwanadamu anafaa kwa kitu chochote mbele ya Mungu? Kwa kweli mwenye hekima anajifaidia mwenyewe tu.


Zamani yeye hakukufalia kitu, lakini sasa atakufalia wewe na mimi vilevile.


kwa sababu hawakumwaminia, wala hawakutumainia kwamba angeweza kuwaokoa.


Mushuhuda mwongo ataangamia, lakini anayejua kusikiliza hawezi kunyamazishwa.


Maandiko Matakatifu yanasema: “Niliamini ndiyo maana nilisema.” Sisi vilevile tunakuwa na imani ile ile, ndiyo maana tunasema.


Nao wakamwambia: “Uko na wazimu!” Lakini akakaza kusema kwamba ni kweli. Basi wakasema: “Ni malaika wake.”


Yule aliyekuwa akiiba, asiibe tena, lakini ajikaze kufanya kazi peke yake kwa usawa kusudi apate kuwasaidia wakosefu.


Basi, ninataka watu waombe Mungu wakiinua mikono juu, ikiwa imetakaswa, nao wafanye vile bila kasirani wala ubishi.


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


na kwa sababu hiyo ninapata mateso haya. Lakini sisikii haya kwa ajili ya ile. Maana ninajua ni nani yule niliyemwamini, nami ninahakikisha kwamba anaweza kuchunga kile alichonipa kwa kunilinda mpaka Siku ile ya kurudi kwake.


Na wewe unapaswa kuwa mufano katika matendo mema, ukionyesha ukweli na heshima katika mafundisho yako.


Tena tushugulikiane kusudi tupate kuvutana sisi kwa sisi kuwa na upendo na kufanya mema.


Akawaambia: ‘Ninyi vilevile muende kutumika katika shamba langu la mizabibu, nami nitawalipa sawa na haki yenu.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite