Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Tito 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 alituokoa sisi. Hakufanya vile kwa sababu ya matendo yetu ya haki, lakini alituokoa kwa sababu ya huruma yake kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetuwezesha kuzaliwa mara ya pili na kuwa na maisha mapya kwa kutusafisha kwa maji.

Gade chapit la Kopi




Tito 3:5
46 Referans Kwoze  

Yeye ndiye aliyetuokoa na kutuita kuwa watu wake, si kwa sababu ya matendo lakini ni kwa sababu ya mupango wake mwenyewe na neema yake aliyotupatia katika kuungana na Kristo Yesu mbele ya nyakati zote.


Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


Maji haya ni mufano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo ule si kwa ajili ya kusafisha uchafu wa mwili lakini ni njia ya kufanya mapatano na Mungu katika zamiri safi. Nao unawaokoa ninyi kwa njia ya ufufuko wa Yesu Kristo,


Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa upendo wake mukubwa;


Alifanya hivi kusudi atakase kanisa kwa ajili ya Mungu, akilisafisha kwa maji na kwa neno.


Unijaze furaha na shangwe, unifurahishe tena, mimi ambaye uliniponda.


Na ikiwa walichaguliwa kwa neema ya Mungu, si kufuatana na matendo. Ingekuwa vile, neema isingekuwa neema tena.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


na kuvaa utu mupya. Utu ule unaendelea kufanywa upya kila mara kufuatana na mufano wa Mungu anayekuwa muumba wake, kusudi mupate kumujua hakika.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Lakini, tunajua kwamba mutu hahesabiwi haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria, lakini kwa njia ya kuamini Yesu Kristo. Sisi vilevile tumeamini Yesu Kristo kusudi tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika yeye, wala si kwa njia ya kushika Sheria. Ni vile kwa maana hakuna mutu atakayehesabiwa haki kwa njia ya kushika Sheria.


Kwa sababu hakuna mutu atakayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa kuwa anatii Sheria, maana Sheria inamusaidia mutu tu kwa kutambua kwamba amefanya zambi.


Zamani ninyi hamukukuwa watu wa Mungu, lakini sasa munakuwa watu wake; zamani ninyi hamukuhurumiwa na Mungu, lakini sasa mumehurumiwa naye.


Inafaa mufanywe upya katika roho zenu na katika nia zenu.


Kwa maana tunaona kama mutu anahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani wala si kwa njia ya kutii Sheria.


Watoto wale walipokuwa hawajazaliwa bado, wala hawajatenda jambo lolote zuri au baya, Mungu alimwambia Rebeka hivi juu yao: “Mukubwa atamutumikia mudogo.” Alisema vile kwa kutimiza mupango wake unaotokana na uchaguzi wake usiofuatana na matendo ya watu, lakini mwito wake kwao.


Kutokana na huruma kubwa ya Mungu wetu, atatutumia mwangaza kutoka juu.


Amesaidia Israeli mutumishi wake, akikumbuka huruma yake,


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako, maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.


Ee Israeli, umutumainie Yawe, maana Yawe ni mwenye wema, naye ana nguvu kubwa ya kutukomboa.


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Lakini wakati Mungu Mwokozi wetu alipoonyesha wema wake na upendo wake kwa watu,


Basi tuseme nini? Watu wa mataifa mengine waliokosa kutafuta kuhesabiwa haki mbele ya Mungu wamehesabiwa haki mbele yake kwa njia ya imani.


Basi mambo hayo, hayatokani na mapenzi ya mutu wala juhudi yake, lakini yanatokana na rehema ya Mungu.


Lakini mutu asipotegemea matendo yake mwenyewe, naye akimwamini Mungu anayemuhesabia mwovu haki, basi imani yake inahesabiwa kuwa haki.


Aliahidi kuwasikilia babu zetu huruma; na kukumbuka agano lake takatifu,


Munafikiri kwamba munafanya sawa, lakini nitayafichua matendo yenu, nayo miungu yenu haitawafalia kitu.


kisha wakianguka, haiwezekani kuwarudisha hata wapate kugeuka mara ingine toka katika matendo yao mabaya. Kwa sababu wamemutundika wao wenyewe Mwana wa Mungu mara ya pili na kumupatisha haya mbele ya watu.


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Mungu amesema mara na mara, nami nimesikia tena na tena kwamba uwezo ni wa Mungu.


Mutu ni nini hata aweze kuwa na moyo safi? Yule aliyezaliwa na mwanamuke atapata kuwa mwenye haki?


Ingawa sina kosa, maneno yangu yenyewe yangenihukumu. Ingawa mimi ni mukamilifu, yangehakikisha kwamba mimi ni mupotovu.


Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Kwa sababu hii ninaweza kuwafanya watu wa taifa langu wawasikilie wivu, hata nipate kuwaokoa wamoja kati yao.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite