Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Tito 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Ujiepushe na mutu anayeleta matengano unapokwisha kumwonya mara mbili.

Gade chapit la Kopi




Tito 3:10
12 Referans Kwoze  

Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.


Mutu akikuja kwenu, naye asipowafundisha mafundisho haya, musimukaribishe ndani ya nyumba yenu, wala musimusalimie;


Kwa inje watajionyesha kama watu wenye kushikamana na ibada, lakini wanazarau uwezo wake. Ujiepushe na watu hao.


Kama mutu hataki kushika maagizo tunayowatolea katika barua hii, mumwangalie vizuri mutu yule, musishirikiane naye, kusudi apate haya.


Wandugu, tunawaagiza katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo kwamba mujitenge na wandugu wote wanaokuwa wavivu na wasiofuata mafundisho tuliyowapa.


kutambikia sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, kasirani, mapingano, matengano, ubaguzi,


Heri wale wanaoleta fujo kati yenu wangejikata viungo vyao vya uzazi.


(Inafaa kuwe matengano kati yenu, kusudi wale wanaokuwa waaminifu wa kweli kati yenu wajulikane.)


Kwa wakati huu ninapokuwa mbali nanyi, ninarudilia kuwaambia waziwazi maneno yale niliyokuwa nimekwisha kuwaambia mbele katika safari yangu ya pili niliyofanya kwenu. Ninawaambia kwamba nitakapokuja kwenu mara tena, sitakosa kuazibu wale waliofanya zambi zamani na wengine wote.


Zamani manabii wa uongo walitokea kati ya watu, na ndivyo hivyo walimu wa uongo watakavyotokea kati yenu. Watu hawa wataingiza mafundisho mabaya sana ya uongo kwa siri, wakimukataa hata Bwana aliyewakomboa na kujiletea maangamizi upesi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite