Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Tito 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Uwaambie wazee wanaume wakuwe wakadirifu, wenye heshima na utaratibu, wenye kukamilika katika imani, katika upendo na uvumilivu.

Gade chapit la Kopi




Tito 2:2
33 Referans Kwoze  

upole na kujizuiza. Hakuna Sheria inayokataza mambo kama hayo!


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Wanawake wao wanapaswa kuwa na adabu vilevile, wasikuwe wasingiziaji wa uongo, lakini wakuwe wakadirifu na waaminifu katika mambo yote.


Mukuwe waangalifu na mukeshe, kwa maana adui yenu Shetani anazungukazunguka kama simba anayenguruma akitafuta yule atakayerarua.


Ushuhuda huo ni wa kweli. Basi kwa hiyo uwaonye vikali, kusudi wapate kuwa na imani kamili.


Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.


Kuwa na imvi za uzee ni taji la utukufu; zinapatikana kwa maisha ya haki.


Lakini sisi ni watu wa muchana, tunapaswa kuwa wakadirifu. Tunapaswa kushikamana na imani na upendo kama vile nguo ya chuma ya kukingia kifua, nalo tumaini letu la wokovu kama vile kofia ya kutulinda.


Kufuatana na neema niliyopewa na Mungu, ninawaambia ninyi wote: mutu asijiwazie kuwa na ukubwa kupita vile inavyomustahili. Lakini mukuwe na mawazo ya ukadirifu, kila mumoja kulingana na kipimo cha imani aliyopewa na Mungu.


Hekima iko kwa watu wazee, maarifa kwa walioishi muda murefu.


Unapokuwa mbele ya muzee unapaswa kusimama kwa kumupa heshima yake, nawe umwogope Mungu wako. Mimi ni Yawe.


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


Mugeuze mafikiri, murudie katika usawa, muache kufanya zambi. Ninasema neno hili kwa kuwapatisha haya, kwa sababu wamoja kati yenu hawamujui Mungu.


Kama miti iliyopandwa katika nyumba ya Yawe, wanastawi katika viwanja vya Mungu wetu;


ukadirifu juu ya elimu yenu, uvumilivu juu ya ukadirifu, kushikamana na ibada juu ya uvumilivu,


Na wewe unapaswa kuwa mufano katika matendo mema, ukionyesha ukweli na heshima katika mafundisho yako.


Lakini inafaa akuwe mwenye kupenda kukaribisha wageni, mwenye kupenda mema, mukadirifu, mwenye haki, mutakatifu na mutaratibu.


Anapaswa kuwa mutu mwenye kuongoza jamaa yake vizuri na kuadibisha watoto wake kusudi wakuwe wenye utii na wenye heshima kabisa.


Shabaha ya agizo hilo ni kusudi kuwe upendo unaotokana na moyo safi na zamiri nzuri na imani ya kweli.


Basi tusilale usingizi kama vile wengine, lakini tukeshe na kuwa wakadirifu.


Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.


Ikiwa kweli tunaonekana kuwa wenda-wazimu, ni kwa ajili ya Mungu, lakini kama sisi ni wenye akili sawa, ni kwa faida yenu.


Na kila mutu anayefanya mashindano katika michezo anajizuiza na vitu vingi katika mazoezi yake. Basi wanafanya hivi kusudi wapate taji yenye kuharibika; lakini sisi tunafanya vile, kusudi tupate taji isiyoharibika.


Lakini Paulo alipokuwa akihubiri juu ya haki, juu ya kujizuiza na juu ya siku ya hukumu ya Mungu itakayokuja, Feliki akaogopa na kumwambia: “Kwa sasa unaweza kujiendea. Nitakuita tena nitakapopata wakati.”


Watu wakakuja kusudi waone jambo lile. Walipofika kwa Yesu, wakamukuta yule mutu aliyetokwa na pepo akiikaa mbele ya Yesu, akiwa amevaa nguo, nayo akili yake ikiwa sawa. Basi watu wale wakaogopa.


Walipomufikia Yesu, wakamwona yule aliyekuwa na kundi la pepo ndani yake akiikaa, akiwa amevaa nguo nayo akili yake ikiwa sawa. Basi watu wale wakaogopa.


Hakutakuwa tena vifo vya watoto wachanga, wazee nao hawatakufa mbele ya wakati wao. Mutu wa miaka mia moja akikufa, amekufa akiwa kijana; na akikufa mbele ya miaka mia moja, ni kusema amelaaniwa.


Vilevile wasaidizi wanaotumika katika kanisa wanapaswa kuwa watu wenye heshima. Hawapaswi kuwa wenye nia mbili katika masemi yao wala wenye kunywa pombe kwa uwingi wala wenye kutafuta mali kwa njia isiyokuwa sawa;


Ninakuandikia wewe Timoteo mwana wangu wa kweli katika imani. Ninakutakia neema na rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.


Sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wanaume wanaozini wao kwa wao, wenye kuuzisha watu, wasema uongo, wale wanaofanya viapo vya uongo na kwa ajili ya wote wanaofanya matendo yanayokuwa umbalimbali na mafundisho ya kweli.


Bwana wetu amenijalia neema kwa uwingi, amenipa imani na upendo tunaokuwa nao katika kuungana kwetu na Kristo Yesu.


Usimukaripie muzee kwa nguvu, lakini umwonye kama baba yako. Uwatendee vijana wanaume kama wandugu zako,


lakini kwa ajili ya upendo, ninapendelea kukusihi, mimi Paulo ninayekuwa muzee, na zaidi sasa ninakuwa mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite