Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Tito 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Nimekuacha katika kisanga cha Krete kusudi upate kutengeneza maneno yaliyobaki na kusimika wazee katika kanisa ndani ya kila muji, ukifuata maagizo niliyokutolea:

Gade chapit la Kopi




Tito 1:5
18 Referans Kwoze  

Wakawachagua wazee katika kila kanisa. Na kisha kuomba na kufunga kula chakula, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana waliyemwamini.


Ukae kule Efeso sawa vile nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia. Na kule uwazuize wale watu wanaofundisha mafundisho ya uongo.


Basi, zaidi ya kuwa na hekima yake, Muhubiri aliendelea kuwafundisha watu ujuzi. Alipima, akachunguza na kutia kwa usawa mezali kwa ufundi mwingi.


Lakini maneno yote yatendeke katika usawa na katika utaratibu.


Wewe umesikia mafundisho niliyotoa mbele ya washuhuda wengi. Nawe sasa uyafundishe kwa watu waaminifu watakaoweza vilevile kuyatoa kwa watu wengine.


Kama mutu akiwa na njaa, akule katika nyumba yake, kusudi musikusanyike kwa kujiletea azabu. Basi maneno mengine yanayobaki nitayatengeneza wakati nitakapofika kwenu.


Watu walikuwa wamepitisha siku nyingi bila kula kitu. Halafu Paulo akasimama mbele yao na kusema: “Warafiki zangu, mungefuata shauri langu na kutoondoka Krete, hamungepata hasara hii na kupoteza vitu kama hivi.


Na kwa sababu kivuko kile hakikukuwa na nafasi zuri ya kukaa wakati wa baridi kali, watu wengi kati yetu wakakubaliana kuondoka kule, kusudi ikiwezekana wafike Foinike, na kupitishia wakati wa baridi kali kule. Foinike ni kivuko kimoja kinachokuwa katika kisanga cha Krete, kinachoelekea upande wa kaskazini-magaribi na wa kusini-magaribi.


Tukasafiri polepole muda wa siku nyingi na kwa shida sana tukafika karibu na muji Kinido. Na kwa sababu upepo ulituzuiza kuendelea mbali ngambo ile, tukapita upande wa kusini wa kisanga cha Krete, kuelekea Salmone.


Nao wakafanya vile, wakatuma misaada waliyokusanya kwa wazee wa kanisa kwa mukono wa Barnaba na Saulo.


Ni nani mungu anayekuwa kama mimi? Muache atangaze na kusema wazi mbele yangu. Nani alitangaza hapo zamani mambo ambayo yatatukia? Watuambie yale ambayo bado yatatokea.


Ijapokuwa mimi ni mbali nanyi kwa mwili, lakini mimi ni pamoja nanyi kwa roho, nami ninafurahi kuona namna munavyoishi katika utaratibu muzuri na kusimama imara katika imani mbele ya Kristo.


kati yao kuna Wayuda na watu waliofuata dini ya Kiyuda, na kuna watu wa inchi ya Krete na ya Arabia. Hata hivi tunawasikia hawa wote wakisema habari za matendo makubwa ya Mungu katika luga zetu za kuzaliwa!”


Upepo usiokuwa mukali ulipoanza kuvuma tokea kusini, wakazani kwamba wataweza tu kutimiza sawa walivyokuwa wamekusudia. Wakapandisha nanga na kuendelea pembenipembeni karibu sana na Krete.


Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.


Na hata mumoja wa manabii wao wenyewe, Mukrete, alisema: “Wakrete ni wasema uongo siku zote, nyama wabaya, wavivu na walafi.”


Kisha watatwaa mawe mapya na kujenga pahali walipobomoa. Nao watapiga nyumba hiyo lipu upya.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite