Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yule ndugu aliyekuwa wa karibu akajibu: “Ikiwa ni hivyo, sitalikomboa shamba hilo, kwa sababu inaonekana kwamba nitauharibu urizi wangu. Afazali nikupe wewe haki yangu ya kulikomboa, maana mimi siwezi kulikomboa.”

Gade chapit la Kopi




Ruta 4:6
8 Referans Kwoze  

Kwa hiyo, kaa hapa usiku wote, na kesho asubui tutaona kama atakubali kukutunza au hapana. Ikiwa atakutunza ni vizuri. Kama vile Yawe anavyoishi, akikataa, mimi nitakutunza. Lala hapa mpaka asubui.”


Kama ndugu yako anakuwa masikini, akiuzisha shamba lake, basi, ndugu yake wa karibu mwenye madaraka ya kulikomboa, atalikomboa.


Lakini kama huyo ndugu wa marehemu hamutaki huyo mwanamuke mujane, basi, mwanamuke huyo atakwenda mbele ya wazee wa muji na kusema: ‘Kaka wa mume wangu marehemu anakataa kuendelesha jina la kaka yake marehemu katika Israeli; hapendi kunitimizia madaraka yake ya kaka wa mume wangu marehemu’.


Basi, Yuda akamwambia Onani: “Umutwae muke wa ndugu yako marehemu, maana vile ndivyo inavyokupasa kufanya, upate kumuzalia ndugu yako watoto.”


Kisha wazee wa muji watamwita huyo mwanaume na kuongea naye. Kama ataendelea kukataa kwamba hataki kumwoa,


huyo mwanamuke mujane atamwendea mbele ya hao wazee wa muji, atamuvua kiatu chake kimoja na kumutemea mate kwenye uso na kumwambia: ‘Hivi ndivyo anavyopaswa kutendewa mutu anayekataa kudumisha nyumba ya kaka yake’.


Basi, Naomi akamwambia mukwe wake: “Yawe amubariki Boazi! Mungu anatimiza siku zote ahadi zake kwa wanaokuwa wazima na waliokufa.” Kisha akaendelea kusema: “Huyo mutu ni ndugu yetu wa karibu na ni mumoja wa wale wenye mapaswa ya kututunza.”


Akauliza: “Wewe ni nani?” Ruta akajibu: “Ni mimi Ruta, mujakazi wako. Kwa sababu wewe ni wa jamaa yangu wa karibu, uitande nguo yako juu ya mujakazi wako.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite