Basi, Yezebeli akaandika barua kwa jina la Ahabu na kuzipiga muhuri wa mufalme. Kisha akapeleka barua hizo kwa wazee na watu wenye heshima walioishi na Naboti kule katika muji.
Ikiwa yule bwana wake alimununua akuwe mumoja wa wake zake, kisha asipendezwe naye, yule bwana ataacha baba ya yule mujakazi amukomboe. Yule bwana hana haki ya kumwuzisha kwa watu wa mataifa mengine, akiwa amemudanganya.
Lakini kama huyo ndugu wa marehemu hamutaki huyo mwanamuke mujane, basi, mwanamuke huyo atakwenda mbele ya wazee wa muji na kusema: ‘Kaka wa mume wangu marehemu anakataa kuendelesha jina la kaka yake marehemu katika Israeli; hapendi kunitimizia madaraka yake ya kaka wa mume wangu marehemu’.