Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 4:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Basi wazee waliokuwa kwenye mulango na watu wote waliokuwa pale wakajibu: “Ndiyo, sisi ni washuhuda. Yawe amufanye muke wako akuwe kama Rakeli na Lea, ambao wote wawili waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe upate kustawi katika jamaa ya Efurata, ukuwe na sifa katika Betelehemu.

Gade chapit la Kopi




Ruta 4:11
24 Referans Kwoze  

Lea akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Rubeni, akisema: “Yawe ameona mateso yangu; bila shaka sasa mume wangu atanipenda.”


‘Ewe Betelehemu, katika inchi ya Yuda, wewe si mudogo kabisa kati ya miji mikubwa ya Yuda, maana ndani yako atatoka mutawala, atakayechunga watu wangu, ndio Waisraeli.’ ”


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Tulisikia wakisema: “Sanduku la Agano ni kule Efurata, tulilikuta katika mashamba ya Yearimu.”


Mutu yule aliitwa Elimeleki na muke wake aliitwa Naomi. Watoto wao wawili wanaume, mumoja aliitwa Malona na mwingine Kiliona. Mutu yule na jamaa yake walikuwa wa kabila la Efuraimu kule Betelehemu katika Yuda. Walikwenda katika inchi ya Moabu, wakakaa kule.


huyo mwanamuke mujane atamwendea mbele ya hao wazee wa muji, atamuvua kiatu chake kimoja na kumutemea mate kwenye uso na kumwambia: ‘Hivi ndivyo anavyopaswa kutendewa mutu anayekataa kudumisha nyumba ya kaka yake’.


Basi, wakamubariki Rebeka wakisema: “Ewe dada yetu! Ukuwe mama wa maelfu kwa maelfu; wazao wako warizi miji ya waadui zao.”


Mwanamuke mwenye hekima anajenga nyumba yake, lakini mupumbafu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.


Efuroni mwenyewe alikuwa kati ya Wahiti hao waliokuwa wamekutanika kwenye mulango wa muji. Basi, Efuroni Muhiti, akamujibu Abrahamu mbele ya Wahiti wote pale kwenye mulango:


Asubui, Yakobo akatambua kwamba ni Lea! Basi, akamwuliza Labani: “Umenitendea jambo gani? Si nilikutumikia kwa ajili ya Rakeli? Mbona basi, umenidanganya?”


Mume wake ni mutu mwenye kuheshimiwa katika baraza, anapoikaa katikati ya wazee wa inchi.


Sasa, Labani alikuwa na wabinti wawili: mukubwa anayeitwa Lea na mudogo anayeitwa Rakeli.


Wana wa Lea walikuwa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuluni.


Wana wa Rakeli walikuwa Yosefu na Benjamina.


Lakini kama huyo ndugu wa marehemu hamutaki huyo mwanamuke mujane, basi, mwanamuke huyo atakwenda mbele ya wazee wa muji na kusema: ‘Kaka wa mume wangu marehemu anakataa kuendelesha jina la kaka yake marehemu katika Israeli; hapendi kunitimizia madaraka yake ya kaka wa mume wangu marehemu’.


Basi, Yezebeli akaandika barua kwa jina la Ahabu na kuzipiga muhuri wa mufalme. Kisha akapeleka barua hizo kwa wazee na watu wenye heshima walioishi na Naboti kule katika muji.


Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu, na Harefu, mwanzilishi wa muji wa Beti-Gaderi.


Nikatia sahihi juu ya barua ya ununuzi, nikaipiga muhuri, nikawaita washuhuda na kuipima ile feza juu ya mizani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite