Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Zaidi ya hayo, nimemupata Ruta wa Moabu mujane wa Malona, kusudi akuwe muke wangu. Mapatano haya yatafanya mali ya jamaa ya marehemu na ukoo wake kubakia kwa watu wake katika muji huu. Ninyi ni washuhuda.”

Gade chapit la Kopi




Ruta 4:10
19 Referans Kwoze  

Mutoto wa kwanza mwanaume atakayezaliwa nao atahesabiwa kuwa wa marehemu kusudi jina lake lisifutwe katika inchi ya Israeli.


Nanyi waume muwapende wake wenu sawa vile Kristo alivyopenda kanisa na kutoa uzima wake kwa ajili yake.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.


Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.


Watu wa Gileadi walikuwa waovu sana; hakuna tena kitu kinachokuwa chao. Kule Gilgali walitambikia ngombe dume. Hivyo, mazabahu zao zitakuwa malundo ya mawe yaliyowekwa kwa mafungu katika shamba.


Basi, nikamupata huyo mwanamuke kwa vikoroti kumi na vitano vya feza na saki nyingi za shayiri.


Wazao wako wangekuwa wengi kama muchanga, kama chembe za muchanga. Jina lao lisingalisahauliwa hata kidogo, wala halingalifutwa mbele yangu.


Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.


Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.


Yawe akumbuke zambi zao siku zote; lakini wao wenyewe wasahauliwe katika dunia.


Yawe anawaangalia watu wa haki, na kusikiliza malalamiko yao;


Basi, Wakanana pamoja na wakaaji wote wa inchi hii watakapopata habari hiyo watatuzunguka na kutufuta kabisa katika dunia. Sasa utafanya nini kwa kuonyesha ukubwa wa jina lako?”


Umutimizie Lea siku zake saba za ndoa, nasi tutakupa Rakeli kwa utumishi wa miaka saba mingine.”


Halafu Boazi akawaambia wazee na watu waliokuwa pale: “Leo ninyi ni washuhuda wangu. Mumeona kwamba nimenunua kutoka kwa Naomi, vyote vilivyokuwa vya Elimeleki, na vya Kiliona na Malona.


Lakini Onani alijua kwamba hao watoto hawangekuwa wake. Kwa hiyo, alipolala na muke wa ndugu yake, alimwanga chini mbegu ya uzazi, kusudi asimupatie ndugu yake watoto.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite