Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Boazi akakwenda kwa nafasi ya kufanyia mukutano kule kwenye mulango wa muji, akaikaa chini. Kisha yule ndugu ya Elimeleki ambaye Boazi alikuwa amemutaja, akapita karibu na pale. Boazi akamwita, akasema: “Kuja, uikae hapa ndugu.” Basi yule mutu akakuja na kuikaa pale.

Gade chapit la Kopi




Ruta 4:1
21 Referans Kwoze  

Ni kweli kwamba ni mapaswa yangu kukutunza, lakini kuna vilevile mwenye mapaswa ya kukutunza na ambaye ni wa karibu zaidi kuliko mimi.


Lakini kama huyo ndugu wa marehemu hamutaki huyo mwanamuke mujane, basi, mwanamuke huyo atakwenda mbele ya wazee wa muji na kusema: ‘Kaka wa mume wangu marehemu anakataa kuendelesha jina la kaka yake marehemu katika Israeli; hapendi kunitimizia madaraka yake ya kaka wa mume wangu marehemu’.


“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Kama nimekunjia yatima ngumi katika tribinali nikijua nitapendelewa na waamuzi,


Nilipokutana na wazee kwenye mulango wa muji na kutwaa nafasi yangu katika mukutano,


basi, mama na baba ya huyo mutoto watamutwaa kumupeleka kwa wazee muji kwenye tribinali.


Basi, nikamwuliza: Unakwenda wapi? Naye akanijibu: Ninakwenda kuupima urefu na upana wa Yerusalema.


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


basi, mumupeleke mutu huyo inje ya miji na kumupiga mawe mpaka akufe.


Efuroni mwenyewe alikuwa kati ya Wahiti hao waliokuwa wamekutanika kwenye mulango wa muji. Basi, Efuroni Muhiti, akamujibu Abrahamu mbele ya Wahiti wote pale kwenye mulango:


Basi, Hamori na mwana wake Sekemu, wakakwenda kwenye mulango wa muji, pahali pa mikutano, wakaongea na watu wao wakisema:


Mwuaji atakimbilia katika muji mumoja wa miji ile na kusimama kwenye mulango wa muji na kuwaelezea wazee wa muji ule maneno yake. Wazee watamupokea ndani na kumupa pahali pa kuishi pamoja nao.


Naye Naomi akasema: “Sasa tulia binti yangu Ruta, mpaka uone litakalotokea. Boazi hatatulia leo mpaka ameyatimiza yote.”


Abusaloma alizoea kuamuka asubui mapema na kwenda kusimama kwenye njia inayoelekea kwenye mulango wa muji. Mutu yeyote aliyekuwa na mashitaki ambayo alitaka kuyapeleka kwa mufalme kwa kupata uamuzi wake, Abusaloma alimwita mutu yule pembeni na kumwuliza: “Unatoka katika muji gani?” Kama mutu yule akisema ametoka katika muji fulani wa kabila la Waisraeli,


Wakati ule, mufalme wa Israeli pamoja na Yosafati, mufalme wa Yuda, walikuwa wameikaa katika viti vyao vya kifalme kwenye kiwanja cha kupepetea ngano kwenye mulango wa kuingilia muji wa Samaria nao walikuwa wakivaa nguo zao za kifalme. Wakati ule manabii wote walikuwa wakitoa unabii wao mbele yao.


Nilipovaa gunia kwa kuomboleza, nikageuka kuwa wimbo kwao.


Mume wake ni mutu mwenye kuheshimiwa katika baraza, anapoikaa katikati ya wazee wa inchi.


Nikatia sahihi juu ya barua ya ununuzi, nikaipiga muhuri, nikawaita washuhuda na kuipima ile feza juu ya mizani.


Wale wamalaika wawili wakafika katika muji wa Sodoma magaribi. Loti alikuwa ameketi kwenye mulango wa muji wa Sodoma. Alipowaona, akasimama kwenda kuwapokea, akainama kwa heshima.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite