Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Boazi alipomaliza kula na kunywa, akachangamuka. Akakwenda karibu na lundo la shayiri, akalala. Ruta akakwenda polepole akafunua miguu yake na kulala pale.

Gade chapit la Kopi




Ruta 3:7
18 Referans Kwoze  

Siku ya saba ya karamu hiyo, mufalme Ahasuero akiwa amejaa furaha kutokana na divai aliyokuwa amekunywa, akawaita matowashi saba waliomutumikia yeye mwenyewe: Mehumani, Bizita, Harbona, Bigita, Abagita, Zetari na Karkasi.


Basi hao watu wawili wakaikaa, wakakula na kunywa pamoja. Kisha baba mukwe akamwambia: “Tafazali, ulale hapa usiku huu na kufurahi.”


Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”


Yule Mulawi na habara yake pamoja na mutumishi wake waliposimama kwenda zao, baba mukwe wake akamwambia yule Mulawi: “Sasa muchana umekwisha na magaribi imekaribia. Ulale hapa, na kufurahi. Kesho asubui utaamuka mapema kuanza safari yako ya kurudi kwako.”


Chakula ni kwa ajili ya kujifurahisha, divai inachangamusha maisha, na feza inasababisha hayo yote.


Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako.


Basi, mimi ninasifu furaha, kwa maana hapa chini ya jua hakuna kitu kinachokuwa kizuri zaidi kuliko kula na kunywa na kujifurahisha. Haya ndiyo mutu anayoweza kufanya anapotoa jasho katika muda wa maisha yake aliyojaliwa na Mungu chini ya jua.


Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,


apate divai ya kumuchangamusha, mafuta ya muzeituni ya kumwangarisha, na mukate wa kumupa nguvu.


Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.


Hapo, Yezebeli, muke wake, akamwambia: “Anayetawala Israeli ni nani? Si ni wewe? Amuka, ukule na uchangamuke. Mimi peke yangu nitakupa shamba la mizabibu la Naboti wa Yezereheli.”


Walipokuwa wanajifurahisha, kumbe wanaume watenda maovu wa muji ule wakakuja wakaizunguka nyumba ile na kugonga kwa mulango. Wakamwambia muzee mwenye nyumba: “Umutoshe inje yule mwanaume aliyekuja kwako, tulale naye.”


Walipojaa na furaha sana ndani ya mioyo yao, wakasema: “Mulete Samusoni atuchekeshe.” Basi wakamutosha Samusoni katika kifungo, wakamuleta naye akawachekesha. Wakamuweka katikati ya nguzo.


Chakula kilikuwa kikitwaliwa kutoka kwenye meza ya Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benjamina alipewa mara tano zaidi ya kipimo wandugu zake walichopewa. Basi, wakakunywa na kufurahi pamoja naye.


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Kwa hiyo, Ruta akakwenda kule katika kiwanja cha kupepetea, akafanya jinsi mama mukwe wake alivyomwamuru.


Katikati ya usiku, Boazi akasisimuka, akageuka, akashituka kumukuta mwanamuke amelala kwenye miguu yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite