Ruta 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Angalia pahali wanapovuna ufuate nyuma yao. Nimewaonya vijana hawa wasikusumbue. Na ukisikia kiu, kwenda kwenye mitungi na ukunywe maji vijana hao waliyoyateka.”
Basi, Mungu akamwambia katika hiyo ndoto: “Sawa. Ninajua kwamba umefanya hivyo kwa moyo safi. Mimi ndiye niliyekuzuia kutenda zambi mbele yangu. Ndiyo maana sikukuruhusu umuguse huyo mwanamuke.
Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”
Halafu Boazi akamwambia Ruta: “Sasa sikiliza binti yangu. Usiende kuokota masuke pahali pengine, lakini katika shamba hili tu. Ushikamane na wanawake hawa.
Hapo Ruta akamwinamia Boazi uso mpaka chini kwa unyenyekevu, akamwambia: “Nimepata namna gani kukubaliwa mbele yako? Mbona unanishugulikia ijapokuwa mimi ni mugeni tu?”