Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 2:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yule kiongozi wa wavunaji akajibu: “Ni binti Mumoabu aliyekuja pamoja na Naomi kutoka katika inchi ya Moabu.

Gade chapit la Kopi




Ruta 2:6
10 Referans Kwoze  

Hivi ndivyo Naomi pamoja na mukwe wake Ruta wa Moabu walivyorudia kutoka Moabu, na wakafika Betelehemu wakati mavuno ya shayiri yalipokuwa yanaanza.


“Basi ni nani anayekuwa mutumishi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kuwa musimamizi wa watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho yao kwa wakati uliopangwa.


Halafu wote wawili wakaendelea na safari mpaka Betelehemu. Walipofika kule, watu wote wakashangaa, hata wanawake wakaulizana: “Huyu ni Naomi?”


Lakini Ruta akamujibu: “Usinisihi nikuache wewe, wala usinizuie kufuatana nawe. Popote utakapokwenda ndipo nami nitakapokwenda, na pale utakapokaa mimi nitakaa, watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.


Basi, Yosefu akapata kukubaliwa mbele ya Potifari, hata akakuwa mutumishi wake wa pekee. Akamufanya musimamizi wa nyumba yake na mwangalizi wa mali yake yote.


Siku moja Abrahamu akamwambia mutumishi wake aliyekuwa muzee kuliko wengine na musimamizi wa mali yake yote: “Weka mukono wako chini ya paja yangu,


Lakini Abramu akasema: “Ee Yawe, utanipa nini wakati ninaendelea kuishi bila mutoto, na murizi wangu ni Eliezeri wa Damasiki?


“Ilipokuwa magaribi, mwenye shamba akamwambia musimamizi wake: ‘Uwaite watumishi na uwalipe mushahara wao, ukianzia kwa wale wa mwisho mpaka kwa wale wa kwanza.’


Kisha Boazi akamwuliza musimamizi wa wavunaji: “Yule binti ni nani?”


Aliniomba nimuruhusu awafuate nyuma wavunaji naye akiokota masalio kati ya miganda. Basi alikuja na amefanya kazi tangu asubui na ni sasa tu amekwenda kupumzika katika kibanda.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite