Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nyuma ya muda, Boazi akafika kutoka Betelehemu, akawasalimia wavunaji, akasema: “Yawe akuwe nanyi.” Nao wakamujibu: “Yawe akubariki.”

Gade chapit la Kopi




Ruta 2:4
21 Referans Kwoze  

Bwana wa amani mwenyewe awape amani siku zote na kwa njia zote. Bwana akuwe pamoja nanyi wote.


Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”


Malaika wa Yawe akamutokea, akamwambia: “Yawe yuko pamoja nawe, ewe shujaa.”


Bwana akulinde. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.


Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Yawe! Tunawabariki kutoka katika nyumba ya Yawe.


Basi wazee waliokuwa kwenye mulango na watu wote waliokuwa pale wakajibu: “Ndiyo, sisi ni washuhuda. Yawe amufanye muke wako akuwe kama Rakeli na Lea, ambao wote wawili waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe upate kustawi katika jamaa ya Efurata, ukuwe na sifa katika Betelehemu.


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


Na wale wanaokuwa na wabwana waamini, wasiwakosee heshima kwa sababu wao ni wandugu. Wanapaswa kuwatumikia vizuri zaidi, kwa maana wao ni wandugu waamini na wapendwa, nao wanashiriki faida ya kazi yao. Hayo ndiyo maneno unayopaswa kufundisha na kuhubiri.


Basi Ruta akaenda katika shamba, akawafuata wavunaji naye akiyaokota masuke waliyoyaacha. Na kumbe akajikuta katika shamba la Boazi, yule wa ukoo wa Elimeleki.


Kisha Boazi akamwuliza musimamizi wa wavunaji: “Yule binti ni nani?”


Mungu Mwenye Nguvu akubariki upate wazao wengi na kuongezeka, kusudi ukuwe jamii kubwa ya watu.


Yawe awabariki na kuwalinda;


Yawe akamwambia: “Nitakuwa pamoja nawe; nawe utawaangamiza Wamidiani sawa vile wangekuwa mutu mumoja.”


Yawe ambaye ameniokoa toka katika makucha ya simba na dubu, ataniokoa kutoka kwa Mufilistini huyu.” Saulo akamwambia: “Kwenda, naye Yawe akuwe pamoja nawe.”


Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu, na Harefu, mwanzilishi wa muji wa Beti-Gaderi.


Yawe akubariki kutoka Sayuni; yeye aliyeumba mbingu na dunia.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitakapowafanikisha tena watu wa Israeli, wao watatangaza tena katika inchi ya Yuda na katika miji yake wakisema: Yawe akubariki, ewe makao ya haki; akubariki, ee mulima mutakatifu!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite