Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Naomi alikuwa na ndugu aliyeitwa Boazi, wa ukoo wa Elimeleki mume wake. Huyo alikuwa mutu mwenye heshima na tajiri.

Gade chapit la Kopi




Ruta 2:1
13 Referans Kwoze  

Salmoni akamuzaa Boazi, Boazi akamuzaa Obedi,


Ni kweli kwamba ni mapaswa yangu kukutunza, lakini kuna vilevile mwenye mapaswa ya kukutunza na ambaye ni wa karibu zaidi kuliko mimi.


Sasa huyu Boazi, ambaye ulifanya kazi na wajakazi wake, si ni wa ukoo wetu? Basi sikiliza, magaribi hii atakuwa katika kiwanja akipepeta shayiri.


Mutu yule aliitwa Elimeleki na muke wake aliitwa Naomi. Watoto wao wawili wanaume, mumoja aliitwa Malona na mwingine Kiliona. Mutu yule na jamaa yake walikuwa wa kabila la Efuraimu kule Betelehemu katika Yuda. Walikwenda katika inchi ya Moabu, wakakaa kule.


sikupata kufurahia wingi wa utajiri wangu au kujivunia mapato mengi ya mikono yangu.


Alikuwa na mali, kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, ngombe elfu moja, punda dike mia tano, na watumishi wengi sana. Yeye alikuwa wa heshima kuliko watu wote kule upande wa mashariki.


Siku moja, Ruta wa Moabu akamwambia Naomi: “Muniruhusu niende kukusanya masalio ya mavuno pahali nitakapopata kukubaliwa na mwenye shamba.” Naomi akamwambia: “Basi, uende binti yangu.”


Menahemu alipata feza hiyo kwa kuwalazimisha watajiri wa Israeli kutoa muchango wa vikoroti makumi tano vya feza kila mumoja. Halafu Puli hakukaa Israeli lakini akarudi katika inchi yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite