Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kisha, Naomi akapata habari kwamba Yawe alikuwa amewabariki watu wake kwa kuwapa chakula. Basi, akaondoka kutoka Moabu kurudi kwao, pamoja na wakwe zake.

Gade chapit la Kopi




Ruta 1:6
27 Referans Kwoze  

Nitaubariki Sayuni kwa mahitaji yake; nitawashibisha chakula wamasikini wake.


Anawapa chakula wenye kumwabudu; hasahau hata kidogo agano lake.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Kwenda uwakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia kwamba: Yawe, Mungu wa babu wao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutokea na kusema: ‘Nimewachunguza ninyi na kuyaona mambo munayotendewa katika inchi ya Misri!


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


“Asifiwe Bwana, Mungu wa Waisraeli, maana amewasaidia watu wake na kuwakomboa.


Utupe chakula chetu cha kila siku.


Yawe anasema hivi: Mutakapopitisha miaka makumi saba huko Babeli, nitawashugulikia na kuitimiza ahadi yangu ya kuwarudisha kwa nafasi hii.


Kama vile mvua na teluji inavyoshuka toka mbinguni, wala hairudi kule lakini inalowanisha udongo, kuuzalisha na kuchipukiza mimea, na kumupatia mupandaji mbegu na kuwapa watu chakula,


Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema.


Yeye anawapatia wanaoonewa haki yao, anawapa wenye njaa chakula. Yawe anawapa wafungwa uhuru,


Viumbe vyote vinakutazamia, nawe unavipatia chakula chao kwa wakati wake.


Yawe alimusikilia Hana huruma naye akajaliwa kupata watoto wa kiume watatu na wabinti wawili. Mutoto Samweli akaendelea kukomaa mbele ya Yawe.


Kisha Yosefu akawaapiza wana wa Israeli, akisema: “Mungu atakapowafikia kwa kuwasaidia, muhakikishe kwamba mutapeleka mifupa yangu kutoka huku.”


Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,


Kisha Yakobo akafanya kiapo akisema: “Ikiwa, ee Mungu, utakuwa pamoja nami na kunilinda katika safari yangu, ukinipa chakula na nguo


Yawe akamukumbuka Sara, akamutendea kama alivyoahidi.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Basi kama tukiwa na chakula na nguo, vile vinatosha.


Analeta amani katika eneo lako; anakushibisha kwa ngano safi kabisa.


Uniondolee uongo na udanganyifu; usinipe umasikini wala utajiri; unipatie chakula ninachohitaji,


Malona na Kiliona nao vilevile wakakufa.


Akaondoka pahali pale alipoishi pamoja na wakwe zake, wakashika njia ya kurudi Yuda.


Wewe utasimama na kurehemu Sayuni, maana wakati umefika wa kuuhurumia, wakati wake uliopangwa umefika.


Alisikiliza, akajibu maombi yao, akasema: Sasa nitawapa tena ngano, divai na mafuta, nanyi mutashiba navyo. Sitawafanya muzarauliwe tena na mataifa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite