Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mutu yule aliitwa Elimeleki na muke wake aliitwa Naomi. Watoto wao wawili wanaume, mumoja aliitwa Malona na mwingine Kiliona. Mutu yule na jamaa yake walikuwa wa kabila la Efuraimu kule Betelehemu katika Yuda. Walikwenda katika inchi ya Moabu, wakakaa kule.

Gade chapit la Kopi




Ruta 1:2
11 Referans Kwoze  

Basi, Rakeli akakufa na kuzikwa kando ya njia inayokwenda Efurata, ni kusema Betelehemu.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Makundi ya waaskari ya Waisraeli na ya Wafilistini walijipanga tayari kupigana vita, makundi yakiwa yanaangaliana uso kwa uso.


Kulikuwa mutu mumoja katika muji wa Rama katika inchi ya milima ya Efuraimu jina lake Elekana wa kabila la Efuraimu. Yeye alikuwa mwana wa Yerohamu, na mujukuu wa Elihu mwana wa Tohu mwana wa Zufu.


Siku hiyo Waisraeli wakawashinda Wamoabu. Inchi ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi nane.


Wakati ule kulikuwa kijana mumoja Mulawi katika muji wa Betelehemu katika inchi ya Yuda.


Lakini Elimeleki, mume wa Naomi, akakufa na Naomi akaachwa na wana wake.


Malona na Kiliona nao vilevile wakakufa.


Naomi alikuwa na ndugu aliyeitwa Boazi, wa ukoo wa Elimeleki mume wake. Huyo alikuwa mutu mwenye heshima na tajiri.


Halafu Boazi akawaambia wazee na watu waliokuwa pale: “Leo ninyi ni washuhuda wangu. Mumeona kwamba nimenunua kutoka kwa Naomi, vyote vilivyokuwa vya Elimeleki, na vya Kiliona na Malona.


Daudi alikuwa mutoto wa Yese, wa ukoo wa Efurata kutoka Betelehemu katika inchi ya Yuda. Yese alikuwa na watoto wanane wa kiume. Wakati Saulo alipokuwa mufalme, yeye alikuwa amekwisha kuwa muzee, mutu mwenye umri mukubwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite