Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ruta 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hapo zamani, wakati waamuzi walipokuwa wanatawala Waisraeli, kulitokea njaa katika inchi. Mutu mumoja kutoka Betelehemu katika Yuda pamoja na muke wake na watoto wao wanaume wawili walikwenda kuishi kwa muda katika inchi ya Moabu kwa kuishi kama wageni.

Gade chapit la Kopi




Ruta 1:1
26 Referans Kwoze  

Wakati ule, njaa ikatokea katika inchi. Njaa hiyo ilikuwa kali, hivyo Abramu akalazimika kwenda Misri kukaa kule kwa muda.


Kisha kukatokea njaa katika inchi ile, nyuma ya ile ya kwanza iliyokuwa kwa wakati wa Abrahamu. Isaka akakwenda Gerari kwa Abimeleki mufalme wa Wafilistini.


Wewe mwanadamu! Taifa fulani likitenda zambi kwa kukosa uaminifu kwangu, mimi nitanyoosha mukono wangu kwa kuliazibu. Nitaiharibu akiba yake ya chakula na kuliletea njaa. Nitawaua watu na nyama wake.


Kijana huyo akaondoka Betelehemu katika inchi ya Yuda, akaenda kutafuta pahali pengine pa kuishi. Katika safari yake akafika katika nyumba ya Mika katika inchi ya milima ya Efuraimu.


Kiburi chenu nitakivunja kabisa kwa kufanya mbingu kule juu kuwa ngumu kama chuma na inchi yenu bila mvua ikuwe ngumu kama shaba.


Kisha njaa ikazidi kuwa kali katika inchi ya Kanana.


Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mungu alileta njaa katika inchi yao, akafunga njia zao zote za kupata chakula.


Mutapanda mbegu nyingi lakini mutavuna kidogo tu kwa sababu nzige watakula mazao yenu.


Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!


Yawe akanitolea mimi Yeremia ujumbe juu ya ule ukosefu wa maji, akisema:


Udongo wenye mboleo akaugeuza kuwa udongo usioweza kutoa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.


Basi, Elia akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huo, njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.


Nyuma ya Yefuta, Ibusani wa muji wa Betelehemu akakuwa mwamuzi wa Israeli.


Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”


Wakati ule kulikuwa kijana mumoja Mulawi katika muji wa Betelehemu katika inchi ya Yuda.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu, na Harefu, mwanzilishi wa muji wa Beti-Gaderi.


Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu alikuwa babu ya: Wanetofati, Waataroti-Beti-Yoabu na nusu ya Wamenahati ni kusema Wazori.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite