Vitisho unavyotoa na kiburi chako vimekudanganya, ewe unayekaa katika mapango ya mawe, unayeishi juu ya kilele cha mulima! Ingawa unaweka makao yako juu kama ya tai, mimi nitakuporomosha kutoka huko unakokuwa. –Ni ujumbe wa Yawe.
Kama mutu anayenyoosha mukono kwenye chicha, ndivyo nilivyokamata mali ya mataifa; kama mutu anayeokota mayai yaliyoachwa ndani ya chicha, ndivyo nilivyoyaokota katika dunia yote. Watu wote walikuwa sawa ndege ambaye hapigi mabawa au kufungua midomo kwa kupiga kelele. Lakini Yawe anasema hivi: