Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Obadia 1:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Wakombozi watapanda juu ya mulima Sayuni kwa kuutawala mulima wa wazao wa Esau; naye Yawe atakuwa ndiye Mufalme.

Gade chapit la Kopi




Obadia 1:21
37 Referans Kwoze  

Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


mukumbuke neno hili: yule anayemurudisha mwenye zambi toka njia ya upotevu ataokoa roho ya yule kutoka kifo, na zambi nyingi zitasamehewa.


Wakati huo, Yawe atakuwa ndiye mufalme pekee wa dunia yote; naye atakuwa ndiye Yawe pekee, mumoja tu, na jina lake litakuwa ndilo jina pekee.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Ujiangalie wewe mwenyewe na kuangalia mafundisho yako, nawe ushikamane nayo. Kwa maana ukifanya hivi, utajiokoa wewe mwenyewe na kuokoa wale wanaokusikiliza.


Ulimwengu wote utakumbuka na kumurudilia Yawe; jamaa zote za mataifa zitamwabudu.


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Mazabahu hayo yatakuwa kitambulisho na ushuhuda kwa Yawe wa majeshi katika inchi ya Misri. Watu wakimulilia Yawe humo kwa sababu ya kugandamizwa, yeye atawapelekea mukombozi atakayewatetea na kuwakomboa.


Halafu Yawe akawapa waamuzi ambao waliwaokoa toka katika mikono ya watu walionyanganya mali zao.


Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.


Kisha nikasikia sauti inayosikilika kama kelele la kundi kubwa la watu, na kama ngurumo ya maporomoko ya maji mengi na kama ngurumo kubwa ya radi ikisema: “Mungu asifiwe! Kwa maana yeye Bwana wetu, Mungu wetu Mwenye Uwezo anatawala.


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Ufalme wako ukuje; mapenzi yako yafanyike katika dunia kama inavyokuwa mbinguni.


Wale wenye hekima watangaa kama vile anga linavyongaa, na wale waliowaongoza wengine kutenda mema, watangaa kama nyota milele.


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Mara moja chuma, udongo wa mufinyanzi, shaba, feza na zahabu, vyote vikavunjika vipandevipande na vikakuwa kama maganda kwenye nafasi ya kupepetea ngano wakati wa jua. Upepo ukavipeperushia mbali wala hakukubakia hata kipande kimoja. Lakini lile jiwe lililoivunja ile sanamu likageuka kuwa mulima mukubwa na kuijaza dunia yote.


Watumishi wako wanapenda muji ule, ijapokuwa ni mabomoko sasa; wanauonea huruma, ingawa umeharibika kabisa.


Yawe akawapa Waisraeli kiongozi ambaye aliwakomboa kutoka kwa Waaramu. Halafu wakakaa kwa amani kama vile walivyokuwa zamani.


Waisraeli wakamulilia Yawe, naye akawapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Otinieli mwana wa Kenazi, ndugu mudogo wa Kalebu.


Hivyo, ukawatia katika mikono ya waadui zao, nao wakawatesa. Lakini wakiwa katika mateso yao, wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa rehema zako nyingi, ukawatumia viongozi wa kuwaokoa; nao wakawakomboa toka katika mikono yao.


Mumwimbie Mungu sifa, mumwimbie! Mumwimbie mufalme wetu sifa, mumwimbie!


Watu wakusifu, ee Mungu, watu wote wakusifu!


Yawe akamwambia: “Mataifa mawili yako ndani ya tumbo lako; makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatatengana. Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine, mukubwa atamutumikia mudogo.”


Maana Yawe ni mufalme; yeye anatawala mataifa.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite