Obadia 1:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200219 Wale wanaokaa Negebu wataurizi mulima wa wazao wa Esau, wale wanaokaa katika Shefela watarizi inchi ya Wafilistini. Waisraeli watarizi inchi za Efuraimu na Samaria na watu wa kabila la Benjamina watarizi inchi ya Gileadi. Gade chapit la |
Watu watanunua mashamba kwa feza, watazitia sahihi barua zake za ununuzi, watazipiga muhuri, na kuweka washuhuda katika inchi ya Benjamina, kandokando ya Yerusalema, katika miji ya Yuda, katika miji ya inchi ya milima, katika miji ya Shefela, na katika miji ya jangwa la Negebu. Maana nitawastawisha tena. –Ni ujumbe wa Yawe.
Basi, Mungu wa Israeli akasukuma roho ya Puli, mufalme wa Asuria, (ambaye alijulikana vilevile kwa jina la Tiglati-Pileseri), akashambulia inchi yao na kuwapeleka watu wa kabila la Rubeni, la Gadi na nusu ya kabila la Manase kwa upande wa mashariki mpaka uhamisho kule Hala, Habori na Hara, pembeni ya muto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.