Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Obadia 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Siku inakaribia ambapo mimi Yawe nitayahukumu mataifa yote. Kama vile mulivyowatendea wengine, ndivyo mutakavyotendewa, mutalipwa kulingana na matendo yenu.

Gade chapit la Kopi




Obadia 1:15
28 Referans Kwoze  

Wewe umenyanganya mataifa mengi, lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Kwa maana mutahukumiwa kufuatana na namna munavyowahukumu wengine, na kipimo kile munachowapimia wengine ndicho kitakachotumiwa kwenu vilevile.


Kwa maana, siku hiyo imekaribia; siku ile ya Yawe iko karibu. Hiyo itakuwa siku ya mawingu ya kutisha, siku ya maangamizi kwa mataifa.


Muwaite wapiga mishale waishambulie Babeli. Mupeleke kila mutu anayejua kuvuta upinde. Muuzunguke muji kusikuwe mutu yeyote atakayetoroka. Muulipize kadiri ya matendo yake yote; muutendee kama ulivyowatendea wengine, maana kwa kiburi ulinizarau mimi Yawe, Mutakatifu wa Israeli.


Ee Babeli, muharibifu wee! Heri yule atakayekulipiza mabaya uliyotutendea!


Ole kwetu kwa ile siku ya Yawe, siku hiyo ya Yawe inakaribia; inakuja pamoja na maangamizi, kutoka kwa Mungu Mukubwa.


kama wewe ulivyofanya wakati inchi ya Waisraeli ilipoharibiwa. Utakuwa jangwa, ewe mulima Seiri, pamoja na inchi yote ya Edomu. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Yawe anasema hivi: Ikiwa wale ambao hawakustahili kunywa kikombe cha azabu ni lazima wakikunywe, basi, wewe utaachwa bila kuazibiwa? Hapana! Hautakosa kuazibiwa; ni lazima ukunywe hicho kikombe!


Adoni-Bezeki akasema: “Wafalme makumi saba waliokatwa vidole gumba vya mikono na miguu waliokota makombo chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa kama nilivyotenda.” Wakamupeleka Yerusalema, akakufia kule.


Mbona Mungu Mwenye Uwezo hapangi wakati wa hukumu? Kwa nini wanaomujua hawajui hizo siku zake?


Kweli, mwangamizaji anashambulia Babeli; waaskari wake wametekwa, pinde zao zimevunjwavunjwa. Mimi Yawe ni Mungu mwenye kuazibu, hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nitakutendea kadiri ya hasira na wivu wako, kulingana na chuki yako kwao. Nitakapokuazibu utatambua mimi ni nani!


Mupige baragumu kule Sayuni; mupige kelele la kujulisha hatari kule juu ya mulima mutakatifu! Mutetemeke enyi wakaaji wa Yuda, maana siku ya Yawe inakuja, siku hiyo iko karibu!


Yawe anaamuru kundi lake kwa sauti; waaskari wake ni wengi sana, wanaomutii hawahesabiki. Siku ya Yawe kweli ni kubwa na ya kutisha sana! Nani atakayeweza kuivumilia?


Ole kwenu ninyi munaoingojea kwa hamu siku ya Yawe! Kwa nini munaitaka sana siku hiyo? Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na si ya mwangaza!


Siku ya Yawe itakuwa giza, na si mwangaza; itakuwa giza kubwa bila mwangaza wowote.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Yawe anasema hivi juu ya jirani wabaya za watu wake: Wamegusa sehemu ya urizi wangu, niliowapatia watu wangu Waisraeli! Basi nitawaongoa kutoka katika inchi yao, na hata watu wa Yuda nitawaongoa katika inchi yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite