Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Obadia 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Hamukupaswa kuangalia tu siku hiyo wandugu zenu walipopatwa na taabu, hamukupaswa kufurahi juu ya Wayuda siku hiyo walipoangamizwa, hamukupaswa kujivuna siku ile wenzenu walipokuwa wanateseka,

Gade chapit la Kopi




Obadia 1:12
27 Referans Kwoze  

Mataifa mengi yamekusanyika kwa kuwashambulia. Yanasema: Muache muji wao uchafuliwe, nasi tufurahie kuona uharibifu wa Sayuni!


kama wewe ulivyofanya wakati inchi ya Waisraeli ilipoharibiwa. Utakuwa jangwa, ewe mulima Seiri, pamoja na inchi yote ya Edomu. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Anayechekelea masikini anamutukana Muumba wake; anayefurahia hasara hatakosa kuazibiwa.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.


Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.


Lakini Yawe anamuchekelea mwovu, kwa maana anajua mwisho wake ni karibu.


Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.


Kundi la waovu limenizunguka; wananizunguka kama kundi la imbwa; wamenitoboa mikono na miguu.


Nimefurahia kuangamia kwa adui yangu, au kufurahi alipopatwa na hasara?


Yule nyama akapewa uwezo wa kusema maneno ya kiburi ya kumutukana Mungu. Naye akapewa mamlaka ya kufanya kazi yake kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.


Hivi vilevile ulimi ni kiungo kidogo cha mwili, lakini unaweza kujivunia mambo makubwa sana. Muangalie, moto kidogo inaweza kuchoma pori kubwa sana!


Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,


Wakaaji wa Edomu, ile inchi ya Uzi, mushangilie na kufurahi kwa sasa. Lakini kikombe hiki cha azabu kitawafikia vilevile. Mutakikunywa na kulewa, hata mutavaa uchi!


Umewatuma watumishi wako kumuchekelea Bwana wenu; wewe umesema: Kwa magari yangu mengi ya vita, nimefika juu kwenye vichwa vya milima, mpaka kwenye vichwa vya milima ya Lebanoni. Nimeangusha mierezi yake mirefu, na misunobari mizurimizuri. Nimevifikia vichwa vyake na ndani ya pori zake kubwa.


Wewe umenipa nguvu kama mbogo; umenimimia mafuta kwa kunifurahia.


Nitakungojea, ewe unayekuwa nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, ni kimbilio langu.


Yeye atawaazibu waadui zangu kwa uovu wao wenyewe; kwa uaminifu wako, ee Mungu, uwaangamize.


Watu wa upande wa magaribi wameshangazwa na yaliyomupata; hofu imewapata watu wa upande wa mashariki.


Lakini mimi nilipoanguka, walikusanyika kunisimanga. Walikusanyika kuniuzi. Wageni nisiowajua walinizomea bila kukoma, wala hakuna aliyewazuia.


Waadui zako wote wanakuzomea, wanakupigia muunzi na kukusagia meno, nao wanasema: Tumemwangamiza! Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu sasa imefika na tumeiona!


Wewe utajua kwamba mimi mwenyewe Yawe nimeyasikia matusi yote uliyoyatoa juu ya milima ya Waisraeli, ukisema: Milima ya Israeli imefanywa kuwa jangwa! Imetolewa kusudi tupate kuinyanganya!


Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wivu wangu unawaka sana. Nitayaazibu mataifa mengine na hasa watu wa inchi ya Edomu. Wao kwa furaha ndani ya moyo na mazarau walikamata hiyo inchi inayokuwa yangu ikuwe yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite