Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Obadia 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kwa sababu ya mateso makali muliyowatendea wandugu zenu wazao wa Yakobo, mutafezeheshwa na kuangamizwa milele.

Gade chapit la Kopi




Obadia 1:10
30 Referans Kwoze  

Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.


Nitakufanya kuwa jangwa milele, na miji yako haitakaliwa tena. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.


Umemuvua madaraka yake ya kifalme, ukauangusha utawala wake chini.


Basi, Esau akamuchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza: “Siku za kilio cha baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.”


Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!”


Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.


Watavaa gunia, hofu itawashika, nao watapata haya na vichwa vyao vyote vitanyolewa.


Wakaaji wa Edomu, ile inchi ya Uzi, mushangilie na kufurahi kwa sasa. Lakini kikombe hiki cha azabu kitawafikia vilevile. Mutakikunywa na kulewa, hata mutavaa uchi!


Ninyi munasema: Tumepatishwa haya na kutukaniwa; haya imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Yawe.


Maana nimeapa kwa nafsi yangu kwamba muji wa Bosira utakuwa kitisho na mushangao, utakuwa uharibifu na kutumiwa kama mufano wa laana; vijiji vyote vitakuwa mabomoko siku zote. –Ni ujumbe wa Yawe.


Sherti tujilaze chini kwa ajili ya haya, na kujiachilia kufunikiwa na haya yetu. Tangu ujana wetu mpaka leo hii, sisi wenyewe, kama vile babu zetu, tumetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wetu, wala hatukumutii Yawe, Mungu wetu.


Waadui zake nitawavalisha haya; lakini yeye nitamuvalisha utukufu wa kifalme.”


Waadui zangu wazungukwe na mazarau; wajifunike haya yao kama vile nguo.


Wanaokutumainia wasifezeheke kwa sababu yangu, ee Bwana wetu, Yawe wa majeshi; wanaokutafuta, wasizarauliwe kwa sababu yangu, ee Mungu wa Israeli.


Lakini Yakobo akamwambia mama yake Rebeka: “Kumbuka kaka yangu Esau amejaa nywele juu ya mwili, lakini mimi sina.


Kwa hiyo, musiwasaidie hao hata kidogo kusudi wapate amani na fanaka.


kwa sababu Waedomu walikuwa wamekuja tena, wakashambulia inchi ya Yuda, wakawashinda na kupeleka wafungwa wengi.


Mwenye haki anajiletea baraka yeye mwenyewe, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.


“Musiwachukie Waedomu; hao ni wandugu zenu. Na musiwachukie Wamisri, maana mulikaa katika inchi yao kama vile wageni.


Anayechekelea masikini anamutukana Muumba wake; anayefurahia hasara hatakosa kuazibiwa.


Yawe anasema hivi juu ya jirani wabaya za watu wake: Wamegusa sehemu ya urizi wangu, niliowapatia watu wangu Waisraeli! Basi nitawaongoa kutoka katika inchi yao, na hata watu wa Yuda nitawaongoa katika inchi yao.


Azabu ya uovu wako, ewe Sayuni imekamilika; Yawe hatawaacha zaidi katika uhamisho. Lakini ninyi Waedomu atawaazibu kwa uovu wenu, atazifichua zambi zenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite