Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wakati ule, walikuwa wamejitenga mbali na watu wa mataifa mengine, wakasimama na kuungama zambi zao na maovu ya babu zao.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 9:2
24 Referans Kwoze  

Watu wa Israeli waliposikia Sheria hiyo wakawatenga watu wa mataifa mengine.


Sasa, mutubu zambi zenu mbele ya Yawe, Mungu wa babu zenu, na kufanya yale yanayomupendeza. Mujitenge na wakaaji wa inchi hii na kuwaacha wake zenu wa kigeni.”


Nikawatakasa watu kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni. Nikatayarisha utaratibu kwa ajili ya makuhani na Walawi juu ya kazi ya kila mumoja wao.


Basi, nilipokuwa nikiomba, nikiitikia zambi zangu na zambi za watu wangu wa inchi ya Israeli, pamoja na kumusihi Yawe kwa ajili ya mulima wake mutakatifu,


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Uniokoe kutoka upanga wa waadui wakali, uniokoe kutoka makucha ya wageni, ambao wanasema maneno ya uongo, wanaonyoosha mukono kwa kushuhudia uongo.


Wayuda wanaoa wanawake wa kigeni na kuwaoea wana wao vilevile. Hivyo, taifa takatifu la Mungu limechanganyika na watu wa mataifa mengine. Vilevile wasimamizi na wakubwa ndio wa kwanza kutenda maovu hayo.”


Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazao wa Yakobo. Maana kweli wachawi kutoka mashariki wamejaa kati yao; kuna waaguzi kama vile kwa Wafilistini. Wanashirikiana na watu wageni.


Unyooshe mukono wako kutoka juu, uniopoe katika maji haya mengi, uniokoe kutoka makucha ya wageni


Usikilize kwa uangalifu maombi yangu, na uniangalie mimi mutumishi wako, ninapokuomba kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli, usiku na muchana. Ninaungama zambi za watu wa Israeli, tulizofanya mbele yako. Mimi pamoja na watu wa jamaa yangu tumefanya zambi.


Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”


kama watakapokuwa kule katika uhamisho wakijifikiri ndani yao wenyewe na kukugeukia, kama katika ile inchi ya uhamisho wakikusihi na kusema ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


Waliokula mwana-kondoo wa Pasaka walikuwa Waisraeli wote waliorudi kutoka katika uhamisho pamoja na watu wengine wote ambao walikuwa wameziacha njia za mataifa mengine kwa kumwabudu Yawe, Mungu wa Israeli.


Nyuma ya mambo haya yote kutendeka, viongozi wakanifikia na kunipa habari hii: “Watu wa Israeli, makuhani na Walawi hawakujitenga na wakaaji wa inchi ambao wanatenda machukizo: Waamoni, Wamoabu na Wamisri, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wayebusi na Waamori.


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Wewe, kubali tu kosa lako: kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako; kwamba chini ya kila muti wenye majani, umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine, wala haukuitii sauti yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Tunakubali uovu wetu, ee Yawe, tunakubali uovu wa babu zetu, maana, tumekukosea wewe.


Sisi wote, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango, waimbaji, watumishi wa hekalu na watu wote waliojitenga na mataifa jirani kufuata sheria ya Mungu pamoja na wake zao, wana wao, na wabinti zao, wote wenye maarifa na ufahamu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite