Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 9:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 lakini wewe kwa rehema zako nyingi haukuwatupilia kule katika jangwa. Nguzo la wingu lililowaongoza muchana, wala nguzo la moto lililowaangazia katika njia usiku, havikuondoka.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 9:19
23 Referans Kwoze  

kwa ajili yao alilikumbuka agano lake, akawahurumia kwa wingi wa wema wake.


Hivyo, ukawatia katika mikono ya waadui zao, nao wakawatesa. Lakini wakiwa katika mateso yao, wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa rehema zako nyingi, ukawatumia viongozi wa kuwaokoa; nao wakawakomboa toka katika mikono yao.


Yawe wa majeshi alisema hivi: Mimi Yawe sibadiliki. Ni kwa sababu hii, ee ninyi wazao wa Yakobo, hamujateketezwa.


Muchana uliwaongoza kwa nguzo la wingu, na usiku uliwaongoza kwa nguzo la moto kwa kuwaangazia njia ya kufuata.


Tega sikio, ee Mungu wangu; angalia uone taabu tunazokuwa nazo na jinsi huo muji unaoitwa kwa jina lako unavyotaabika. Tunakutolea maombi yetu si kwa sababu tumetenda haki, lakini kwa sababu wewe una huruma nyingi.


Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na musamaha, ingawa sisi tumekuasi.


watawapasha wakaaji wa inchi habari hii. Maana watu hawa wamekwisha kupata habari kwamba wewe, ee Yawe, uko pamoja nasi; maana wewe, ee Yawe, unaonekana waziwazi wingu lako linaposimama juu yetu, na kwamba wewe unatutangulia muchana kwa nguzo ya wingu na usiku kwa nguzo ya moto.


Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.


Wema wa Yawe haukomi, huruma zake hazina mwisho.


Yawe anasema hivi: Ewe Israeli, watu wa Yakobo, kumbuka kwamba wewe ni mutumishi wangu. Nilikuumba kusudi ukuwe mutumishi wangu, nami sitakusahau hata kidogo.


Hata hivyo, kutokana na rehema zako nyingi, haukuwaachilia waangamie kabisa au kuwatupilia, maana wewe ni Mungu mwenye huruma na rehema.


Katika safari zao zote, Waisraeli waliweza kuliona lile wingu la Yawe juu ya hema wakati wa muchana na ule moto ukiwaka juu yake usiku.


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


Katika safari zao zote Waisraeli hawakuanza safari hata kidogo isipokuwa wakati wingu hilo lilipoinuliwa kutoka juu ya hema.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


Aliongoza watu wake katika jangwa. Wema wake unadumu milele.


Lakini nikawaonea huruma, sikuwaangamiza kule katika jangwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite