Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 9:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Wakakataa kutii; hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao. Wakakuwa wagumu, wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha katika utumwa katika inchi ya Misri. Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe, mwenye huruma na rehema, haukasiriki upesi, uko mwema sana. Haukuwatupilia

Gade chapit la Kopi




Nehemia 9:17
43 Referans Kwoze  

Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Kwa maana anamwambia Musa: “Nitamuhurumia yule ninayependa kumuhurumia; nitamurehemu yule ninayependa kumurehemu.”


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Mimi nitakaa kati ya wazao wa Waisraeli, na sitawaacha hata kidogo watu wangu, Waisraeli.”


Babu zetu walipokuwa Misri, hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu; hawakukumbuka wingi wa wema wake, lakini walimwasi kando ya bahari Nyekundu.


Walisahau mambo aliyokuwa ametenda, ndiyo miujiza aliyokuwa amewaonyesha.


Yawe, Mungu wetu, akuwe nasi kama alivyokuwa na babu zetu. Tunaomba asituachilie, wala asitutupilie.


Lakini bila kukawia walisahau matendo yake, wakaacha kutegemea shauri lake.


Lakini kwako tunapata usamehe, kusudi sisi tukuheshimu.


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


“Babu zetu hawakutaka kumusikiliza Musa, wakamukataa na kutamani kurudi Misri.


“Nimewaita nanyi mumekataa kusikiliza, nimewanyooshea mukono mukuje nanyi hamukujali,


Zaidi ya hayo, haukutuleta katika inchi inayotiririka maziwa na asali, wala kutupatia urizi wa mashamba na mashamba ya mizabibu. Unafikiri utawafanya hawa watu kuwa vipofu? Hatutakuja!


Lakini Musa akasema: Sasa mbona munavunja agizo la Yawe? Hivyo hamutashinda!


Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?


Hata hivyo, kutokana na rehema zako nyingi, haukuwaachilia waangamie kabisa au kuwatupilia, maana wewe ni Mungu mwenye huruma na rehema.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Mimi nitaleta juu ya muji huu na juu ya vijiji vyote vinavyokuwa kandokando yake hasara zote nilizotangaza juu yake, kwa sababu wakaaji wake ni wenye mioyo migumu, nao wamekataa kusikia maneno yangu.


Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.


Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na musamaha, ingawa sisi tumekuasi.


Yawe hakasiriki upesi, lakini amejaa nguvu, Yawe hatawaachilia wenye makosa hata kidogo. Yawe anapopita, upepo mukali na zoruba vinatokea; mawingu ni mavumbi yanayonyanyuliwa na miguu yake.


Ninawafahamu watu hawa. Wao wana vichwa vigumu.


Lakini, kwa hayo yote, wanapokuwa katika inchi ya waadui zao, mimi sitawatupa wala kuwachukia hata kuwaangamiza kabisa na kuvunja agano langu.


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.


Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.


Hawakushika agano la Mungu; walikataa kufuata sheria yake.


Lakini hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini wakazidi kufanya vichwa vyao kuwa vigumu na kuasi kuliko hata babu zenu.


Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanaifukizia miungu ya uongo ubani. Wamejikwaa katika njia zao, wameacha barabara zao za zamani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite