Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 9:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri, watumishi wake wote na watu wote wa inchi yake; maana ulijua kwamba waliwagandamiza babu zetu. Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 9:10
32 Referans Kwoze  

Na sasa ee Bwana, Mungu wetu, uliyewaondoa watu wako katika inchi ya Misri kwa nguvu yako kubwa na kulifanya jina lako litukuzwe mpaka sasa, tunasema kwamba tumetenda zambi; tumefanya maovu.


Katika inchi ya Misri ulifanya maajabu, ukatenda miujiza, na unaendelea kufanya hivyo mpaka leo kati ya Waisraeli na katika mataifa mengine vilevile, jambo ambalo limekufanya ujulikane kila nafasi.


Kama vile ngombe wanavyopelekwa kwa kulishwa katika bonde, ndivyo Roho wa Mungu alivyowapumzisha watu wake. Ndivyo, ee Mungu ulivyowaongoza watu wako, nawe ukajipatia jina tukufu.


ambaye kwa mukono wake wenye nguvu alifanya maajabu kwa njia ya Musa, akapasua bahari na kuwaongoza watu wake, na kujipatia jina la milele?


Kuna Mungu yeyote mwingine aliyejaribu hata kidogo kwenda kujitwalia taifa lake kutoka taifa lingine, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyofanya, kwa kutumia majaribio, vitambulisho, maajabu, vita, na vitisho? Hapana. Lakini mulishuhudia kwa macho yenu namna Yawe alivyofanya kwa mukono wake wenye nguvu kabisa kule Misri.


Sasa ninajua kwamba Yawe ni mukubwa kuliko miungu yote, maana amewakomboa watu hawa toka katika mikono ya Wamisri ambao waliwatendea ubaya.”


Lakini mufalme wa Misri akawauliza: “Ni nani yule Yawe, hata nimusikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simujui yule Yawe, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.”


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Mungu anamwambia mufalme wa Misri katika Maandiko Matakatifu: “Nimekusimika kuwa mufalme kwa sababu hii moja, ni kusudi kwa njia yako nipate kuonyesha uwezo wangu na kusudi jina langu lipate kutangazwa katika dunia yote.”


Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.


Yawe akamwambia Musa: “Mimi ninakufanya kuwa kama mungu kwa mufalme wa Misri, naye ndugu yako Haruni atakuwa nabii wako.


Kwa hiyo nitaunyoosha mukono wangu na kupiga inchi ya Misri kwa maajabu ambayo nitayafanya kule. Kisha mufalme atawaacha muondoke.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Lakini wao na babu zetu wakakuwa na kiburi na wakakuwa wagumu wakakataa kufuata maagizo yako.


Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako, hata hivyo, kwa kiburi chao, wakaacha kutii amri zako. Wakaasi maagizo yako, ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi. Wakakuwa wenye kiburi vilevile wakakuwa wagumu, na wakakataa kuwa watiifu.


Mukumbuke ugonjwa mukali muliouona kwa macho yenu, miujiza na maajabu na nguvu kubwa na uwezo mukubwa, ambavyo Yawe, Mungu wenu alitumia kwa kuwakomboa; vile ndivyo atakavyowatendea watu munaowaogopa.


Ninyi mumeona mambo mengi, lakini hamuelewi kitu. Masikio yenu yako wazi, lakini hamusikii kitu!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite