Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Ezra akamushukuru Yawe, Mungu mukubwa na watu wote wakaitikia: “Amina! Amina!” nao wakiwa wakiinua mikono yao juu. Kisha wakamwabudu Mungu nazo nyuso zao zikigusa chini.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 8:6
30 Referans Kwoze  

Basi, ninataka watu waombe Mungu wakiinua mikono juu, ikiwa imetakaswa, nao wafanye vile bila kasirani wala ubishi.


Tumufungulie Mungu mioyo yetu na kumwomba kule juu mbinguni:


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Kisha mufalme Yosafati akainama uso mpaka chini pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema na kumwabudu Yawe.


Na wamalaika wote waliokuwa wakizunguka kile kiti cha kifalme, wazee na vile viumbe vine vya ajabu, wakainama uso mpaka chini mbele ya kiti cha kifalme, nao wakamwabudu Mungu,


Muinue mikono kuelekea pahali patakatifu, na kumutukuza Yawe!


Nikakunguta upindo wa kanzu yangu na kusema: “Kila mumoja asiyetimiza ahadi hii Mungu amukungute, amutoe katika nyumba yake na katika kazi yake. Basi, akungutike na kubaki mikono mitupu.” Mukutano muzima wakaitikia, na kusema: “Amina”; wakamusifu Yawe. Watu wakafanya kama vile walivyokuwa wameahidi.


Halafu yule mutu akainamisha kichwa chake, akamwabudu Yawe


Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


ninyi mutawajibu: ‘Hii ni sadaka ya Pasaka kwa Yawe, kwa sababu alipita nyumba za Waisraeli katika inchi ya Misri. Aliwaua Wamisri, lakini sisi hakutuua.’ ” Waisraeli wakainamisha vichwa na kumwabudu Yawe.


Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Kwa maana kama ukimwomba Mungu ndani ya roho tu kwa kumushukuru, mutu asiyeelewa kitu anayehuzuria katika mukutano hawezi kusema amina kwa kuitikia maombi yako ya kushukuru. Ni kwa sababu hasikii mambo unayosema.


Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Ikuwe hivyo! Yawe afanye hivyo. Yawe ayatimize maneno uliyotabiri, avirudishe hapa vyombo vya nyumba ya Yawe kutoka Babeli pamoja na watu wote waliohamishiwa huko.


Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


Wema wako ni bora kuliko maisha. Nitakusifu kwa midomo yangu.


Wewe unaniimarisha katika ukamilifu; utanichunga mbele yako milele.


Sikiliza sauti ya ombi langu, ninapokulilia unisaidie, ninapoinua mikono yangu kuelekea hekalu lako takatifu.


Kisha mufalme Hezekia na viongozi wakawaambia Walawi wamusifu Yawe kwa nyimbo ambazo mufalme Daudi na nabii Asafu walizotunga. Basi, watu wote wakamutukuza Mungu kwa furaha, na kuinama uso mpaka chini.


Akasema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, maana kwa nguvu zake ametimiza ahadi yake aliyoitoa kwa baba yangu Daudi akisema:


Lakini Abramu akamwambia mufalme wa Sodoma: “Ninaapa kwa Yawe, Mungu Mukubwa, aliyeumba mbingu na dunia,


Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele! Kisha watu wote wakasema: “Amina!” Wakamusifu Yawe vilevile.


Walawi hawa ndio walisaidia kuwaelewesha watu Sheria: Yesua, Bani, Serebia, Yamini, Akubu, Sabetayi, Hodia, Maasea, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya; na kila mumoja akiwa akisimama pale alipokuwa.


Halafu Daudi akamutukuza Yawe mbele ya mukutano wote, akisema: “Utukuzwe milele na milele, ee Yawe, Mungu wa baba yetu Israeli.


Sasa, nimeamua ndani ya moyo wangu kufanya agano na Yawe, Mungu wa Israeli, kusudi asitukasirikie zaidi.


Maana Yawe ni Mungu mukubwa; yeye ni mufalme mukubwa juu ya miungu yote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite