Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 7:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mungu akanipa moyo kuwakusanya viongozi na watu kwa kujua ukoo zao. Nikapata kitabu cha ukoo za watu waliorudi toka katika uhamisho mara ya kwanza, na hawa ndio waliokuwa wameandikwa ndani yake.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 7:5
15 Referans Kwoze  

Wandugu zangu wapendwa, musidanganyike!


Ni kwa sababu hiyo ninatumika na kupigana kwa uwezo ninaopewa na Kristo, unaoniwezesha kufanya kazi kwa nguvu.


Shukrani kwa Mungu aliyemutia Tito bidii ya kuwasaidia kama vile sisi tunavyokuwa nayo!


Si kusema kwamba sisi wenyewe tuko na uwezo wa kujitungia jambo hili, lakini uwezo wetu unatoka kwa Mungu.


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.


Hao walitafuta kitabu cha vizazi vyao kati ya wengine walioandikwa katika kitabu cha ukumbusho za ukoo, lakini ukoo wao haukuonekana. Kwa hiyo hawakuruhusiwa kutiwa katika kazi ya ukuhani maana walihesabiwa kuwa wachafu.


Nikamwomba Mungu nikisema: “Ee Mungu, kumbuka mambo yote Tobia na Sanibalati waliyotenda, hata yule Noadia, nabii mwanamuke, na manabii wengine waliotaka kuniogopesha.”


Sasa, Ee Mungu wangu, kumbuka wema wangu wote niliowatendea watu hawa.


Ezra akasema: “Asifiwe Yawe, Mungu wa babu zetu, ambaye amemupatia mufalme moyo wa kupamba nyumba ya Yawe inayokuwa Yerusalema.


Hao walitafuta ukoo wao katika kitabu cha ukoo, lakini hawakuonekana humo. Kwa hiyo hawakuruhusiwa kushika ukuhani maana walihesabiwa kuwa wachafu.


Muji wa Yerusalema ulikuwa mupana na mukubwa, lakini wakaaji wake walikuwa wachache na nyumba zilikuwa hazijajengwa.


Maana Yawe anawapa watu hekima; katika kinywa chake kunatoka maarifa na ufahamu.


Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite