Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 6:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Waadui zetu katika mataifa jirani, waliposikia kwamba kazi tumeimaliza, wakaogopa na kupata haya sana; maana walijua hakika kwamba kazi hii ilikamilika kwa musaada wa Mungu wetu.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 6:16
16 Referans Kwoze  

Wafalme wote wa Waamori walioishi ngambo ya magaribi ya Yordani, na wafalme wote wa Wakanana waliokuwa kandokando ya bahari ya Mediteranea, waliposikia kwamba Yawe aliyakausha maji ya muto Yordani kwa ajili ya Waisraeli mpaka walipokwisha kuvuka, wakavunjika moyo; wakaishiwa nguvu kabisa kwa kuwaogopa Waisraeli.


Hapo kinywa chetu kilijaa kicheko; tulishangilia kwa furaha. Nao watu wa mataifa mengine walisema: “Yawe amewatendea mambo makubwa!”


Hivyo, kwenye sehemu za chini za ukuta ambazo zilikuwa bado kumalizika, nyuma ya ukuta, katika pahali pa wazi, nikawapanga watu kulingana na jamaa zao wakiwa na mapanga, mikuki na pinde.


Lakini Sanibalati, Tobia, Waarabu, Waamoni na Waasidodi waliposikia kwamba ujenzi mupya wa ukuta wa Yerusalema ulikuwa unasonga mbele na kwamba nafasi zilizobomoka katika ukuta zimezibwa, wao walizidi kukasirika.


Lakini Sanibalati wa muji wa Muhori na Tobia, Mwamoni, mutumishi wake, waliposikia kwamba nimekuja kwa kushugulikia hali njema ya watu wa Israeli, hawakufurahia kabisa jambo hilo.


Na sasa mimi ninawashauria ninyi, musiwafuatilie watu hawa, muwaache wajiendee. Kwa maana ikiwa mupango huu na hii kazi yao vimeanzishwa na mwanadamu, sherti vitaharibika.


Hakika ulozi hauwezi kuwapinga watu wa Yakobo, wala uchawi juu ya watu wa Israeli. Sasa juu ya Israeli, watu watasema: Muangalie maajabu Mungu aliyotenda!


Alikwamisha magurudumu ya magari yao, yakakuwa yakienda kwa shida sana. Halafu Wamisri wakasema: “Tuwakimbie Waisraeli! Yawe anawapigania Waisraeli mbele yetu.”


Wakati ule wote, viongozi wa Wayuda walikuwa wakiandikiana na Tobia.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


akawaambia: “Mimi ninajua kwamba Yawe amewapa inchi hii; tumepatwa na hofu juu yenu na wakaaji wote wa inchi hii wanatetemeka kwa sababu yenu.


Mara tu tuliposikia mambo hayo, tukavunjika moyo kabisa kwa sababu yenu, tukaishiwa nguvu kabisa. Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu juu mbinguni na chini katika dunia!


Uwaonyeshe watu kuwa wewe ndiwe uliyetenda hayo. Wewe, ee Yawe, ndiwe uliyefanya hivyo.


Wafezeheke na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia Sayuni.


Yawe anajenga tena Yerusalema; anawarudisha Waisraeli waliopelekwa katika uhamisho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite