Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 5:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Watawala walionitangulia walikuwa muzigo muzito kwa watu wakiwadai chakula na divai. Zaidi ya hiyo waliwalipisha vikoroti makumi ine vya feza. Hata watumishi wao waliwatesa watu. Lakini, mimi sikufanya hivyo, maana nilimwogopa Mungu.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 5:15
19 Referans Kwoze  

Kisha nikawaambia: “Jambo munalofanya si zuri. Haiwapasi kumwogopa Mungu wetu kwa kuzuia mataifa mengine yanayokuwa waadui zetu yasituzarau?


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Kwa wema na uaminifu mutu anaondoa uovu. Kwa kumwogopa Yawe anaepuka ubaya.


Wakati nilipokuwa kwenu, sikumulemea mutu yeyote nilipohitaji kitu fulani, kwa maana wandugu waliotoka Makedonia waliniletea vitu vyote nilivyohitaji. Nilijiangalia vizuri katika mambo yote kusudi nisiwalemee, nami nitaendelea kujiangalia vema.


Na kama mukiwasalimia wandugu zenu tu, munatenda tendo gani la kupita wengine? Hata wapagani wanatendeana vile!


Maana hasara kutoka kwa Mungu ni kitisho kwangu; mimi siwezi kusimama mbele ya ukubwa wake.


Mumepungukiwa na nini kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi sikuwalemea kwa kupata musaada toka kwenu? Munisamehe kwa kosa hili.


Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


Atatwaa sehemu ya kumi ya ngano zenu na ya zabibu zenu na kuwapa wakubwa wake na watumishi wake.


Abrahamu akamujibu: “Nilifanya hivyo kwa sababu hakuna anayemwogopa Mungu pahali hapa na kwamba mungeniua kusudi mumutwae muke wangu.


Siku ya tatu Yosefu akawaambia: “Kwa sababu ninamwogopa Mungu, mufanye hivi kusudi mupate kuishi:


Nilikuwa na juhudi nyingi katika ujenzi mupya wa ukuta huu na sikujipatia hata shamba. Hata watumishi wangu wote walifanya kazi hii kwa bidii.


Nikalinunua shamba hilo linalokuwa kule Anatoti, kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nikamulipa bei yake vikoroti kumi na saba vya feza.


Watumwa wanatutawala, wala hakuna wa kutuokoa toka katika mikono yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite