Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Nikakunguta upindo wa kanzu yangu na kusema: “Kila mumoja asiyetimiza ahadi hii Mungu amukungute, amutoe katika nyumba yake na katika kazi yake. Basi, akungutike na kubaki mikono mitupu.” Mukutano muzima wakaitikia, na kusema: “Amina”; wakamusifu Yawe. Watu wakafanya kama vile walivyokuwa wameahidi.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 5:13
17 Referans Kwoze  

Lakini wakati Wayuda walipingana naye na kumutukana, kwa hiyo akakunguta mavumbi yaliyorukia juu ya nguo zake na kuwaambia: “Lazima ya kuazibiwa kwenu ikuwe juu ya kichwa chenu wenyewe! Mimi sina kosa. Tangu sasa nitawaendea watu wa mataifa mengine.”


Na katika nyumba au muji wowote watakapokataa kuwakaribisha na kukataa kusikiliza maneno yenu, mutakapotoka kule mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu.


Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele! Kisha watu wote wakasema: “Amina!” Wakamusifu Yawe vilevile.


Halafu hawa mitume wakawakungutia mavumbi toka juu ya miguu yao, na kwenda katika muji Ikonio.


Angalia kinywa chako kisikuingize katika zambi, halafu ikupase kumwambia mujumbe wa Mungu kwamba haukukusudia kutenda zambi. Kwa nini kumusukuma Mungu akukasirikie na kuiharibu kazi yako?


Nimeapa na kuhakikisha kiapo changu, kwamba nitashika maamuzi yako ya haki.


Kasirani ya watu inasababisha tu sifa yako; walioponyoka katika vita watafanya sikukuu zako.


Shukrani ikuwe ndiyo sadaka yako kwa Mungu. Umutimizie Mungu Mukubwa ahadi zako.


Ezra akamushukuru Yawe, Mungu mukubwa na watu wote wakaitikia: “Amina! Amina!” nao wakiwa wakiinua mikono yao juu. Kisha wakamwabudu Mungu nazo nyuso zao zikigusa chini.


Halafu mufalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri zake, maagizo na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakaungana katika kufanya agano.


Halafu Samweli akamwambia Saulo: “Tangu leo Yawe ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako na atamupa mutu mwingine kati ya wajirani zako anayekuwa bora kuliko wewe.


Maji haya yanayoleta laana yaingie ndani ya tumbo lako na kukufanya tasa na tumbo lako livimbe. Naye mwanamuke ataitikia: Amina! Amina!


Kwa maana kama ukimwomba Mungu ndani ya roho tu kwa kumushukuru, mutu asiyeelewa kitu anayehuzuria katika mukutano hawezi kusema amina kwa kuitikia maombi yako ya kushukuru. Ni kwa sababu hasikii mambo unayosema.


Watu wanaovunja sheria wanasifu waovu, lakini wanaoshika sheria wanapingana nao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite